Trending Videos
Title: Nandy - Kivuruge (Official Video)
2 months ago
Zanzibar 2401Jan
Dk: Shein asisitiza kudumishwa amani na utulivu visiwani Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wananchi wa Zanzibar kuendelea kuidumisha hali ya amani na utulivu ambayo ndio msingi wa mafanikio yanayoendelea kupatikana hivi sasa na yatakayopatikana hapo baadae.
Dk. Shein ameyasema hayo leo katika risala yake ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2019 aliyoitoa kupitia vyombo vya habari, Ikulu mjini Zanzibar.
Dk. Shein amesema kuwa katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya mwaka 2018 mafanikio makubwa yamepatikana ambayo yamechangiwa na kuwepo kwa amani, mshikamano, umoja na mapenzi yaliopo.
Katika risala yake hiyo Dk. Shein alieleza kuwa hali ya amani, umoja na mshikamano uliopo nchini ni jambo muhimu linalowavutia Washirika wa maendeleo ambao wanaridhika na jitihada zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ndio maana wanaiunga mkono katika mipango yake ya maendeleo.
Amesema kuwa hapana shaka kwamba iwapo amani, usalama na utulivu vitadumishwa na kufanya kazi kwa bidii Washirika wa Maendeleo watakuwa pamoja na Zanzibar katika kuisaidia ili kuweza kutekeleza malengo yaliyopangwa.
Rais Shein alitoa shukurani kwa wananchi wote kwa kuunga mkono juhudiza serikali za kuiletea maendeleo Zanzibar na kueleza kuwa moyo wao huo wa umoja na mshikamano umewezesha kuimarisha vizuri hali ya uchumi wa Zanzibar.
Hata hivyo, Dk. Shein alitoa shukurani nyingi kwa wananchi wote kwa kuunga mkono juhudi za Serikali za kuiletea maendeleo Zanzibar ambapo moyo wao huo wa umoja na mshikamano umewezesha kuimarisha vizuri hali ya uchumi wa Zanzibar.
“Tukiwa tunaukaribisha mwaka mpya wa 2019, nachukua fursa hii kwa niaba ya wananchi wote wa Zanzibar kuwashukuru kwa dhati Washirika wetu wa Maendeleo kwa kuendelea kutuunga mkono, tunathamini mikopo, misaada na ushauri tulioupata kutoka kwao”, alisema Dk. Shein.
The post Dk: Shein asisitiza kudumishwa amani na utulivu visiwani Zanzibar appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
Zanzibar 2401Jan
Naibu Katibu Mkuu mpya aahidi kusimamia kwa vitendo katiba ya CCM

NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Zanzibar Ndugu Othman Ally Maulid akizungumza mara baada ya kukabidhiwa Ofisi rasmi katika hafla iliyofanyika leo katika Afisi Kuu ya Wazazi Kikwajuni Unguja.
NAIBU Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Ndugu Othman Ally Maulid amesema atasimamia kwa vitendo ibara ya Tano ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo jipya la mwaka 2017 inayoelekeza kuwa Ushindi wa CCM ni lazima kwa kila Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Chaguzi ndogo ndogo na Uchaguzi Mkuu.
Kauli hiyo ameitoa leo katika Hafla ya makabidhiano ya Ofisi baina yake na Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Mhe. Najma Giga huko katika Afisi ya Wazazi iliyopo Mpirani Kikwajuni Zanzibar.
Ndugu Othman amesema kwamba pamoja na majukumu mbali mbali ya kiutendaji yanayoikabili Jumuiya hiyo bado ana jukumu la msingi la kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi kinashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Ameeleza kuwa kila Taasisi nchini ina malengo yake hivyo kwa upande wa CCM ambayo ni taasisi ya Kisiasa ni lazima iwekeze mipango yake katika kuhakikisha inashinda na kuendelea kuongoza wananchi kwa misingi ya uadilifu.
Katika hafla hiyo Naibu Katibu Mkuu huyo ameahidi kushirikiana na Watendaji, Viongozi na Wanachama wote wa Jumuiya na Chama kwa ujumla ili kuleta ufanisi wa kiutendaji ndani ya Jumuiya hiyo.
Aidha amewasisitiza viongozi na watendaji wa Jumuiya hiyo kuvitumia vyombo vya Habari nchini kutangaza miradi mbali mbali inayotekelezwa na Serikali chini ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Dkt.John Pombe Magufuli.
Katika maelezo yake Naibu Katibu Mkuu huyo amesema atatumia miongozo mbali mbali ya CCM na Jumuiya ya Wazazi kubuni mipango mbali mbali ya maendeleo itakayosaidia kuleta ufanisi.
Naye Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa Wazazi Najma Giga, amewashukru viongozi na watendaji wote wa jumuiya ya wazazi kwa ushirikiano waliompa wakati wote alipokuwa kiongozi wa Taasisi hiyo.
Aliwasisitiza Watendaji wa Taasisi hiyo kushirikiana vizuri na Naibu Katibu mpya ili kuendeleza mafanikio yaliyopo ndani ya Jumuiya hiyo.
Aidha ameeleza kuwa licha ya kumaliza muda wake wa kiuongozi ndani ya Jumuiya hiyo bado ataendelea kuwa karibu katika kushiriki masuala mbali mbali ya kimaendeleo ndani ya Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya hiyo.
Akitoa shukrani Mkuu wa Utawala msaidizi Ndugu Mustafa Rashid, amesema kwa niaba ya watendaji wenzake watafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Naibu Katibu Mkuu huyo ili kufikia malengo endelevu yaliyowekwa na jumuiya hiyo katika kuimarika kisiasa, kiuchumi na kijamii.
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
The post Naibu Katibu Mkuu mpya aahidi kusimamia kwa vitendo katiba ya CCM appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
Zanzibar 2401Jan
Magazeti ya Tanzania Leo Jumanne January 1, 2019
Kama kawaida Zanzibar24 tayari imeshakusogezea stori kubwa zilizotengeneza headline katika kurasa za mbele na nyuma za Magazeti ya Tanzania Leo Jumamosi January 1, 2019. Chukua time yako kwa kupitia Stori zote kali za udaku, siasa, michezo, burudani na mambo mengine mbali mbali.



















The post Magazeti ya Tanzania Leo Jumanne January 1, 2019 appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
MwanaHALISI01Jan
Watoto 5,500 watazaliwa 2019, UNICEF wajipanga kwa usalama wao
2 months ago
MwanaHALISI01Jan
Serikali yaanika hali ya uchumi nchini
2 months ago
VOASwahili01Jan
Brazil kufungua ubalozi Jerusalem
2 months ago
VOASwahili01Jan
Uchaguzi wa Rais DRC 2018: Wananchi wajitokeza kupiga kura
2 months ago
VOASwahili01Jan
Tanzania : Waziri Mhagama, Mkuu wa SSRA watakiwa kuwajibika
2 months ago
RFI
Uhusiano kati ya Tanzania na jumuiya ya kimataifa matatani
2 months ago
RFI
MSF: Maambukizi ya Malaria yapungua katika kambi ya wakimbizi ya Nduta nchini Tanzania
2 months ago
RFIMuseveni amtaka rais wa Burundi kuzungumza na wapinzani wake
2 months ago
RFI
Spika wa bunge la Afrika Mashariki azuru Zanzibar
2 months ago
RFI
Khawar Qureshi kusimamia kesi za ufisadi zinazowahusu viongozi mashuhuri Kenya
2 months ago
Malunde
SERIKALI YATOA MAAGIZO KWA WAMILIKI WA VITUO VYA AFYA NA MAABARA BINAFSI

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Tiba wa Wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto na Mkurugenzi wa bodi ya usajili wa maabara Dkt. Dorothy Gwajima amesema kuwa hadi kufikia Septemba 2018 bodi ya usimamizi wa maabara binafsi ilitambua jumla ya maabara 641 zinazojitegemea na maabara 719 zilizoshikizwa kwenye vituo vya tiba vya watu binafsi vya ngazi mbalimbali.
Amesema kuwa kutokana na baadhi ya wamiliki wa maabara binafsi hasa zilizoshikizwa kutofuata maadili ya uwajibikaji kisheria kufikia Septemba 20, bodi kupitia ziara yake imebaini kuwa kati ya vituo vya tiba 1731vya watu binafsi vyenye maabara ndani ni maabara 1012 sawa na asilimia 58 pekee ndizo zilizotimiza wajibu wake wa kujiandikisha kwenye bodi ya usimamizi wa maabara binafsi na kutekeleza matakwa ya kisheria.
Amesema kuwa wamiliki ambao hawatatekeleza wajibu wao wa kumiliki maabara hizo watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kifungo pamoja na faini au vyote kwa pamoja.
Amewataka wamiliki hao kuhakikisha kuwa kila mmoja awe amekidhi vigezo vyote vya umiliki wa maabara ikiwa ni pamoja na kulipa ada zote stahiki zikiwemo malimbukizo ya nyuma na faini stahiki pamoja na kuwa na risiti halali za malipo hayo. Pia amewataka wamiliki wa maabara hizo kulipa tozo stahiki kila mwaka ili kuwezesha bodi kufanya uhakiki wa kudumu wa huduma zitolewazo katika maabara hizo.
Vilevile amesema kuwa katika kutekeleza hilo watatoa orodha za zahanati katika gazeti la Serikali na zahanati isiyokuwapo kwenye orodha hiyo haitatakiwa kutoa huduma yoyote na watakaokiuka watakutana na mkono wa dola. Gwajima ametoa mwito kwa serikali katika ngazi zote kushirikiana na kutoa taarifa dhidi ya wavunja sheria na kufanikisha kuipeleka mbele sekta hiyo.
Akieleza kuhusiana na faini zitakazotolewa Kaimu Afisa msajili wa bodi ya usimamizi ya maabara binafsi Neema Halliye amesema kuwa kwa mujibu wa sheria watakaokiuka sheria hiyo watapigwa faini ya kulipa kiasi cha shilingi laki mbili au kufungwa miaka miwili au vyote kwa pamoja na bado maboresho ya sheria hiyo yanafanyiwa kazi ili kuweza kutoa kibano zaidi.
2 months ago
Malunde
ZITTO KABWE AANIKA ORODHA YA VITABU 49 ALIVYOSOMA MWAKA 2018

Vitabu vingine huwa vitabu rejea na huvirudia kwa ajili ya mafunzo ili kufanya maamuzi Fulani Fulani au kwa ajili ya ibada (kwa mfano Quran) au kwa sababu nyenginezo. Nafurahi kuwa hivi sasa kwenye mitandao duniani kote watu wamekuwa wakiorodhesha vitabu ili kujengana katika utamaduni wa kusoma. Barack Obama yeye alianza kuweka orodha yake mwaka 2015 na tayari ameshaweka orodha ya mwaka huu. Obama pia huweka orodha ya muziki aliyopenda mwaka huo. Inavutia.
Mwaka huu nimesoma vitabu 49 (kutoka vitabu 36 + 3 vya mwaka 2017). Wakati natoa orodha yangu 23/12/2017 nilikuwa bado nasoma riwaya za Jumba Maro ya Ally Saleh na The Feast of the Goat cha Mario Vargos Llosa ambazo nilizimaliza nikiwa Maputo, Msumbiji.
Pia niliweza kuongeza Simulizi iitwayo Zeitoun ya Dave Eggers kuhusu kimbunga cha Katrina huko New Orleans, Marekani. Hii ni simulizi ya wahamiaji kutoka Syria walivyoshiriki kuokoa makumi ya watu kutoka kwenye maafa ya Hurricane Katrina.
Mwaka 2018 nimesoma mchanyato kidogo kuliko mwaka 2017 ambapo dhima (themes) kadhaa ziliniongoza. Hata hivyo bado njaa yangu ya kuwasoma madikteta duniani iliendelea kuniongoza kwa lengo la kupata ufahamu na maarifa ya namna ya kuchangia katika kuzuia nchi yetu kuangukia kwenye utawala wa Imla. Pia nilijaribu kutafuta majawabu ya changamoto hizo. Kwenye dhima hiyo nilisoma:
- The Death of Democracy: Hitler’s Rise to PowerBenjamin C Hett
- The Plots Against HitlerDanny Orbach
- Franco: Anatomy of a DictatorEnrique Moradiellos
1 The New Sultan: Erdogan and the Crisis of Modern TurkeyOner Cagaptey
- How Democracies DieD Ziblatt and S Levitsky
Kama nilivyopata kusema, ninapenda na kujivunia sana historia ya ukombozi dhidi ya ukoloni barani Afrika na haswa Ukombozi wa Kusini mwa Afrika.
Mwaka huu niliongeza maarifa katika eneo hilo kwa kusoma sio tu habari nzuri za vyama vya ukombozi bali pia baadhi ya makosa waliyofanya viongozi wetu. SWAPO Captive kilichoandikwa na Bwana Angula ni simulizi muhimu sana kusoma ili kuona namna baadhi ya watu walivyoonewa kwenye harakati za ukombozi. Kwa jina la ukombozi watu huonewa, huteswa na hata huuwawa. Pia nilisoma kuhusu mashujaa wa ukombozi na athari kwa familia zao. Katika dhima hii ya Ukombozi nilisoma:
- Cuito Cuanavale: 12 Months of War That Transformed a ContinentFred Bridgland
- Africa TomorrowEdem Kadjo
- Umkontho we Sizwe: The ANC Armed StruggleThula Simpson
- Mozambique: Sowing the Seeds of RevolutionSamora Machel
- 491 DaysWinnie Mandela
- Thabo MbekiAdekeye Adebajo
- Umkontho we SizweJanet Cherry
- Chris HaniHugh Macmillan
- Being Chris Hani’s DaughterLindiwe Hani and Melinda Ferguson
- SWAPO Captive: A Comrade’s Experience of Betrayal and TortureOiva Angula
Pia nilisoma vitabu vya hali ya sasa ya Afrika Kusini baada ya ukombozi:
- No Longer Whispering to Power: The Story of Thuli MadonselaThandine Gqubule
- How to Steal A City: The Battle for Nelson Mandela Bay, An Inside AccountCrispian Olver
- How to Steal A Country? State Capture and Hope for the Future in South AfricaRobin Renwick
- Coalition Country: South Africa After the ANCLeon Schreiber
Kama Mtanzania ninayejiandaa kwa majukumu muhimu ya kitaifa nimekuwa nikipenda kupata maarifa Zaidi kuhusu Historia ya Zanzibar. Mwaka 2018 niliongeza maarifa kwa kusoma vitabu kadhaa ikiwemo:
- The Threat of Liberation: Imperialism and Revolution in ZanzibarAmrit Wilson
- Social Memory, Silenced Voices and Political Struggle: Remembering the Revolution in Zanzibar.(Ed) W. Cunningham and M. Fouere
Vitabu vinavyofuata ni mchanyato wa riwaya, historia za watu na mataifa mengine, mafunzo ya uchumi na kadhalika. Vitabu vinavyohusu Marekani na utawala wao mpya chini ya Trump ni kwa lengo la kujifunza nini kinaendelea huko. Kitabu cha Deng Xiaoping nilipewa na ndugu yangu Harith Ghassany katika mjadala wa kisomi wa kutafuta modeli sahihi ya kimaendeleo kwa nchi zetu za Afrika.
- Pakistan: Personal StoryImran Khan
- Making Africa Work: A Handbook for Economic SuccessGregg Mills, O Obasanjo, et al
- SidetrackedHenning Mankell
- In Praise of Blood: The Crimes of Rwandan Patriotic FrontJudi Rever
- Thomas Sankara SpeaksThomas Sankara
- A Higher LoyaltyJames Comey
- State Secrets: Deathly High Stakes in the Corridors of PowerQuintin Jardine
- Deng Xiaoping and The Transformation of ChinaEzra F Vogel
- Gorbachev: His Life and TimesWilliam Taubman
- Tell TaleJeffrey Archer
- The Growth DelusionDavid Pilling
- CTRL ALT DELETE: How Politics and The Media Crashed Our DemocracyTom Baldwin
- Unhinged: An Insider’s Account of The Trump White HouseOmarosa Manigault
- Fire and Fury: Inside The Trump White HouseMichael Wolf
- Why The Dutch are DifferentBen Coates
- The French Revolution: What Went WrongStephen Clarke
- An Extra Ordinary Life: A Passion for ServiceV J Mwanga
- Uwajibikaji Ndani ya Kalamu Isiyokuwa na WinoLudovich Utouh
- Betting the House: Inside Story of the 2017 ElectionsTim Ross and Tom McTaguwe
- In Defence of BolsheviksMax Shachtman
- The Future That Works: Selected Writings of A M Babu(Ed) Salma Babu and Amrit Wilson
- Our Commonwealth: The Return of Public Ownership in USAThomas Hanna
- Democracy, Direct Action and Socialism: A Debate of FundamentalsMichael Foot and Sean M
Mwaka huu ukiwa unaelekea ukingoni, Wachapishaji wa Vitabu Mkuki na Nyota Publishers walichapisha upya vitabu vya harakati za Willy Gamba, mpelelezi maarufu barani Afrika. Rafiki yangu katika kusoma vitabu Fadhy Mtanga (ambaye pia ni adui yangu kwenye soka – maana yeye ni shabiki mandazi wa Manchester United FC na mimi shabiki wa mabingwa watarajiwa Liverpool FC) alininunulia vitabu vyote 4 vya Mzee Elvis Musiba. Nilikuwa na muda wa kutosha na kuvisoma vyote bila kuweka chini. Namshukuru sana Fadhy kwa zawadi yake murua kabisa. Vitabu hivi ni:
- Kikosi Cha KisasiA E Musiba
- NjamaA E Musiba
- Kufa na KuponaA E Musiba
- HofuA E Musiba
Kitabu changu cha mwisho mwaka 2018 ni :
- Dear Ijeawele OR A Feminist Manifesto in 15 SuggestionsChimamanda Adichie
Vitabu 3 vilivyonigusa sanaThe Death of Democracy: Hitler’s rise to power cha Benjamin Hett kilinigusa sana kutokana na namna wanasiasa wanavyoweza kufanya makosa yenye kudidimiza nchi kwa sababu tu ya kulinda madaraka. Katika kitabu hiki somo kubwa ni namna Wabunge wa vyama vyote vya Siasa walivyomruhusu Adolf Hitler kutunga sheria inayompa mamlaka makubwa wakiamini kuwa Hitler ana nia njema na atawalinda.
Wabunge wa Chama cha SDP ndio pekee walikataa, walizomewa, kuzodolewa na hata kuuwawa. Wengine walikimbilia uhamishoni. Ndani ya miezi michache, hata wale waliomwunga mkono Hitler walishughulikiwa na Taifa la Ujerumani likaingia kwenye taharuki kubwa na hatimaye vita vya pili vya dunia.
Waliompa madaraka Hitler waliamini kuwa watamdhibiti. Hawakuweza. Historia kama hii ipo lakini wanaadam hatujifunzi tunarudia makossa hayo kila wakati katika nchi mbalimbali duniani.
How Democracies Die cha Ziblatt na Levitsky kilinigusa sana kwa kuwa kinatoa majawabu ya changamoto za demokrasia kuanguka. Licha ya kwamba ni kitabu maalumu kwa muktadha wa nchi ya Marekani, kitabu hiki nilicholetewa na rafiki yangu Rakesh Rajani, kinatazama mifano ya nchi mbalimbali duniani kama Colombia na njia walizotumia kuhami demokrasia (walitumia sana Bunge na Mahakama), Venezuela (jinsi mgomo wa vyama vya upinzani kutoshiriki chaguzi ulivyotoa nafasi ubwete kwa chama tawala) na hata Ujerumani ambayo hali yake nimeeleza hapo awali.
Somo kubwa kabisa kutoka kitabu hiki ni kwamba ni lazima wadau wote wa demokrasia kushirikiana pamoja kupambana na udikteta bila kujali tofauti ndogo ndogo au kubwa kubwa miongoni mwao. Bila ushirikiano dikteta husaga saga kila mmoja. Ni Kitabu nashauri kila mwana demokrasia akisome.
Dear Ijeawele Or A Feminist Manifesto in 15 Suggestions cha Chimamanda Adichie ni kitabu kidogo sana kwa idadi ya kurasa. Kwa hakika ni barua ambayo Chimamanda kamwandikia rafikiye ambaye amepata mtoto wa kike na anamshauri amkuze vipi mtoto huyu. Kijitabu hiki kimenigusa kwa sababu kinatoa changamoto kadhaa kwa sisi wanaume katika malezi.
Kuna mambo ambayo tunafanya tunaona kama ni msaada kumbe inapaswa kuwa wajibu kwa familia. Kwa mfano, mara nyingi husikia wanaume tukisema ‘leo nafanya kazi ya kulea mke wangu kasafiri’ ama kwa kimombo ‘baby-sitting’. Chimamanda anatuambia hapa, Baba mtoto hafanyi ‘baby-sitting’ bali anatimiza wajibu wake kama baba. Pia kinachoitwa ‘gender roles’ kwenye nyumba zetu kiasi kwamba tunazuia watoto wa kike kukua na kukuza vipawa vyao vyote.
Nashauri wenye watoto wa kike wasome kijitabu hiki, wababa na wamama kwani kinaweza kuchangia kubadili mtazamo wako wa namna tunalea watoto wetu wa kike. Mapendekezo 15 ya Chimamanda unaweza usiyakubali yote lakini yana mafunzo mengi ambayo yanaweza kukufaa kwenye malezi ya mabinti zetu.
Heri ya Mwaka mpya 2019
Zitto KabweDar es Salaam30/12/2018
2 months ago
Malunde
SERIKALI YATOA UFAFANUZI KUHUSU SAKATA LA MWANANCHI KUKAMATWA AKISAFIRISHA VITANDA VIWILI

Afisa huyo alikuwa akitekeleza majukumu hayo kwa mujibu wa kifungu cha 93 (Powers of officers with respect to offences) inayompa mamlaka Afisa Misitu au Afisa wa Jeshi la Polisi kukagua, kukamata na kuzuia mazao yanayodhaniwa kupatikana kinyume na sheria.
Kufuatia taarifa hizo, uongozi wa TFS umefanya uchunguzi wa haraka na kubaini kuwa abiria mmoja alikuwa akisafirisha vitanda viwili (2) vipya kwa basi. Vitanda hivyo vililipiwa ushuru wa Serikali kupitia mfumo wa Kielektroniki wa Malipo Serikalini (GePG) na kupewa stakabadhi halali ya tarehe 26 Disemba, 2018 katika kituo cha Mkata, Handeni Mkoani Tanga.
Katika kutekeleza majukumu yake, Afisa wetu alimtaka abiria huyo kuonesha Hati ya Kusafirishia (Transit Pass) bidhaa hizo kwa mujibu wa Kanuni ya 13(4) ambayo inakataza mwenye chombo chochote cha usafiri kusafirisha mazao ya misitu ambayo hayana hati ya usafirishaji ambapo abiria huyo hakuwa nayo.
Hata hivyo, Afisa wetu alishindwa kutafsiri masharti ya kifungu hiki na mahitaji ya utoaji wa Hati ya Usafirishaji kwani kama msafirishaji binafsi kwa matumizi ya nyumbani asingeweza kukidhi vigezo vya kuwa na hati hiyo.
Hati ya Usafirishaji huhitaji msafirishaji kuonesha usajili, leseni ya biashara, utambulisho wa mlipa kodi na namba ya usajili wa chombo kinachotumika kusafirisha mazao hayo pamoja na kuonesha vituo atakavyopaswa kukaguliwa.
Kufutia tukio hilo, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unamwomba radhi abiria huyo na umma wa watanzania kwa tukio hilo na usumbufu uliojitokeza. Wakala unaendelea kufuatilia suala hili, na utahakikisha kuwa tukio kama hili halijirudii tena.
Aidha, hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa mujibu wa Kanuni za utumishi wa umma dhidi ya mtumishi aliyehusika na utoaji wa lugha isiyo na staha wakati akitekeleza sheria ya misitu ambapo alitegemewa kutoa elimu stahiki kwa umma. Hivyo, TFS inapenda kufafanua mambo yafuatayo:- 2
1. Kwamba ikiwa mwananchi yeyote amenunua samani mpya kutoka kwa watengenezaji au wauzaji mahali popote kuhakikisha anapatiwa risiti halali kwa malipo aliyofanya. Hivyo, mmiliki wa samani mpya kwa matumizi binafsi halazimiki kuwa na Hati ya Usafirishaji anaposafirisha toka eneo moja kwenda jingine isipokuwa awe tayari kuonesha uthibitisho wa nyaraka za malipo halali ya samani hizo kwa ukaguzi pale itakapohitajika.
2. Mwananchi yeyote anayesafirisha samani zilizotumika kutoka eneo moja hadi jingine halazimiki kuwa hati za malipo wala kuwa na hati ya kusafirishia samani hizo.
3. Serikali itaendelea kufanya mapitio ya Sheria ya Misitu na Kanuni zake ili kuepuka mkanganyiko wowote wa tafsiri ya sheria unaoweza kujitokeza na kuondoa usumbufu kwa wananchi.
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unapenda kutoa rai kwa wananchi wote kuendelea kuzingatia Sheria za uhifadhi wa misitu. Aidha, Wakala hauna nia ya kuzuia utengenezaji, usafirishaji na matumizi ya samani za mbao mahali popote nchini ilimradi tu upatikanaji wa malighafi zake uwe umefuata utaratibu. Lengo ni kuhakikisha kuwa rasilimali za misitu zinatunzwa na kutumika kwa njia endelevu kwa maendeleo ya Taifa. Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania utaendelea kutoa elimu kwa umma pamoja na watumishi wake kuhusu taratibu za uvunaji, usafirishaji na biashara ya mazao ya misitu nchini kupitia njia mbalimbali na kuhakikisha huduma bora kwa wananchi.
IMETOLEWA NAKITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO KWA UMMAWAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA (TFS)
2 months ago
Malunde
CCM WAANIKA SIFA ZA WAGOMBEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2019

Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amesema atakayejihusisha na vitendo vya rushwa katika mchakato wa chama hicho tawala kusaka wagombea wake katika uchaguzi wa Serikali za mitaa, atapoteza sifa za kugombea.
Ametoa kauli hiyo leo Jumapili Desemba 30, 2018 alipokutana na wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya za Muleba na Biharamulo mkoani Kagera.
Amesema kila kiongozi wa CCM atakayejitokeza kugombea uenyekiti wa kijiji au mtaa, lazima awe mwadilifu na mwaminifu.
Amebainisha kuwa baadhi ya wagombea wanatumia majukwaa kupinga rushwa licha ya kuwa wanajihusisha nayo, ikiwa ni pamoja na kukiuka maadili ndani ya chama.
"Makatibu wa CCM kila ngazi hata nyie msiwe wa kupokea rushwa kupitisha majina ya wagombea wasiokuwa na sifa lazima kiongozi afuate miiko na ahadi za mwanachama,” amesema Bashiru.
ENDELEA KUSOMA HAPANa Shaaban Ndyamukama, Mwananchi
2 months ago
CHADEMA Blog
2 months ago
CHADEMA Blog
2 months ago
CHADEMA Blog
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Yanga yawaacha Ajib na Makambo kombe la Mapinduzi
Kuelekea michuano ya kombe la Mapinduzi inayoanza kesho Januari 1, 2019 visiwani Zanzibar, klabu ya Yanga haitapeleka kikosi chake cha kwanza kwenye mashindano hayo.
Kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya Yanga kimeeleza kuwa baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza wamepewa mapumziko na kocha Mwinyi Zahera ili kujiweka sawa kwaajili ya mechi za ligi kuu.
”Badala ya kwenda na kikosi cha kwanza mwalimu ameeleza kuwa Yanga itakwenda na wachezaji ambao wamekuwa hawapati nafasi ili nao waweze kucheza na kujenga uwezo wa kujiamini’‘, kimeeleza chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa.
Miongoni mwa wachezaji ambao hawatakwenda ni kinara wa mabao wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu, Heritier Makambo, pamoja na Ibrahim Ajib na wachezaji wengine.
Katika michuano hiyo ambayo inatarajiwa kufikia tamati Januari 13, Yanga imepangwa kwenye Kundi B na timu za KVZ, Malindi, Jamhuri, Azam na Yanga.
The post Yanga yawaacha Ajib na Makambo kombe la Mapinduzi appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Manara awashtaki Yanga Mamlaka ya mapato’TRA’
Msemaji wa Klabu ya Simba, ambao pia ni Mabingwa Watetezi, Haji Manara amehoji Mamlaka ya mapato Tanzania juu utaratibu wa watani zao wa jadi kuhusu kuchangisha kwa ajili ya klabu yao na kuuliza kama utaratibu huo ni sahihi.
Manara amehoji iwapo kama Klabu hiyo inayoongoza msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara kama inalipia kodi katika Mamlaka hiyo huku akisistiza kwamba hata kama ukweli ukiwa mchungu kiasi gani lazima usemwe.
“TRA nakumbuka mlienda katika kanisa la Mchungaji Kakobe kufuatilia ile michango na zile sadaka za waumini, Vipi kwa hawa wanaochangisha kila uchwao? wana mashine za EFD? wanalipia kodi za hizi Rambirambi za kujitakia?”, ameandika Manara.
“Nategemea ‘soon’ (mapema) wahusika watatoa maelekezo sahihi ya huu utamaduni unaotufedhehesha Watanzania na ambao ukiachwa unaweza kusababisha kizungumkuti cha kukokotoa hesabu”. Manara amesema katika kusisitiza kauli yake.
The post Manara awashtaki Yanga Mamlaka ya mapato’TRA’ appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
VOASwahili01 Jan
2 months ago
Malunde01 Jan
MANARA AWAINGIZA YANGA MTEGONI

Manara amehoji iwapo kama Klabu hiyo inayoongoza msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara kama inalipia kodi katika Mamlaka hiyo huku akisistiza kwamba hata kama ukweli ukiwa mchungu kiasi gani lazima usemwe.
"TRA nakumbuka mlienda katika kanisa la Mchungaji Kakobe kufuatilia ile michango na zile sadaka za waumini, Vipi kwa hawa wanaochangisha kila uchwao? wana mashine za EFD? wanalipia kodi za hizi Rambirambi za kujitakia?", ameandika Manara.
Katika kusisitiza kauli yake, Manara amesema "Nategemea 'soon' (mapema) wahusika watatoa maelekezo sahihi ya huu utamaduni unaotufedhehesha Watanzania na ambao ukiachwa unaweza kusababisha kizungumkuti cha kukokotoa hesabu".
2 months ago
Michuzi
WANACHAMA WA YANGA KWA KAULI MOJA WAKUBALI MABADILIKO

Wanachama wa Yanga kwa kauli moja wamfikia hatua ya makubaliano kwenda katika mfumo wa mabadiliko ambao utaruhusu timu hiyo kuwa Kampuni.Yanga iliyofanya mkutano wake jana Jijini Dar Es Salaam, ulianza kwa hotuba ya Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe na kuwaasa wanachama wa Yanga wafanye maamuzi sahihi ili kuweza kuiweka timu yao katika dira nzuri.Dkt Mwakyembe amesema kuwa Yanga ni alama ya ukumbusho barani Afrika kama klabu iliyoweza kusaidia upatikanaji wa uhuru wa Tanganyika na bara la Afrika."Yanga imechaguliwa kuwa alama ya ukumbusho barani Afrika kama moja ya vilabu vilivyobeba alama ya uhuru wa Tanganyika na uhuru wa bara la Afrika, Yanga ni klabu kubwa na yenye historia yake ndania ya nchi hii , "amesema Dkt Mwakyembe.Dkt Mwakyembe amesema uwekezaji katika klabu za mpira ni jambo lisilokwepeka na hata serikali inaunga mkono suala hilo kulingana na mahitaji yanayohitajika ili kuwa na soka la ushindani.Pia amesema wanachama waacheni kuichukulia mzaha mzaha tu na kufikia inafungwa mpaka na timu ndogo ila maamuzi yao ndiyo yatakayoamua mustakabali wa timu ya Yanga.Pia katika mkutano huo wanachama waliweza kupinga barua ya kujiuzulu kwa mwenyekiti wao Yusuf Manji na kusema kuwa bado wanamtambua kama mwenyekiti mpaka sasa hivi.Wanachama hao wamesema kuwa hawawezi kukubaliana na baria hiyo na wamemuomba arejee katika nafasi yake ya Uenyekiti wa klabu yao ambapo wka kipindi cha mwaka mmoja imekua imekaimiwa na Makamu mwenyekiti Clement Sanga.
Ikumbukwe kuwa Mwaka 2017, Manji aliandika barua ya kujiuzulu nafasi yake katika klabu ya Yanga ila ndani ya mwaka mzima Yanga haikuwahi kuweka mkutano wa wanachama ili kuweza kuijadili barua hiyo.Baada ya kupinga suala la kujiuzulu Manji anarejea Yanga akiwa mwenyekiti huku akisaidiwa na Makamu mwenyekiti Clement Sanga.
2 months ago
BBC
Liverpool 5-1 Arsenal: Pierre-Emerick Aubameyang has just 13 touches against Reds
2 months ago
BBC
Stanley Kwenda: Why football stars have Congo on their mind
2 months ago
BBCSwahili
Manchester United itamenyana na Liverpool siku ya Jumapili.
2 months ago
BBCSwahili
Manchester United: Ole Gunnar Solskjaer ateuliwa kuongoza Mashetani Wekundu baada ya Mourinho kutimuliwa, kusaidiwa na Mike Phelan
2 months ago
BBCSwahili
Callum Wilson: Bournemouth na Chelsea wavutania mchezaji anayechezea timu ya taifa ya England
2 months ago
BBCSwahili
Jurgen Klopp: Kocha wa Liverpool asema Chelsea na Arsenal wangali katika mbio za ubingwa
2 months ago
BBCSwahili
Jedwali la Msimamo wa ligi ya EPL 2018/19: Manchester City, Man United, Liverpool, Chelsea, Arsenal
2 months ago
BBCSwahili
Pep Guardiola: Liverpool huenda ndio bora zaidi duniani kwa sasa, asema mkufunzi wa Man City
8 months ago
Malunde10 Jun
GOR MAHIA WAIPA KICHAPO SIMBA SC...SAFARI YA LIVERPOOL BASI TENA

Game ya fainali ilichezwa katika uwanja wa Afraha Nakuru nchini Kenya lakini kikubwa ukiachilia mbali zawadi ya Kombe na pesa, zawadi ya Bingwa kwenda katika jiji la Liverpool England katika uwanja wa Goodson Park iliongeza hamasa na mvuto wa game yenyewe.
Bahati mbaya Simba ambao ndio walikuwa wawakilishi pekee wa Tanzania katika mchezo huo wa fainali, wamejikuta wakipoteza nafasi ya kucheza na Everton baada ya kukubali kipigo cha magoli 2-0, hivyo Gor Mahia wanatetea Ubingwa wao na watacheza tena kwa mara ya pili game ya kirafiki na Everton.
Kingine kilichokuwa kinaleta mvuto ni kuwa Simba SC ilikuwa inacheza na Gor Mahia ambayo inafundishwa na kocha Dylan Kerr raia wa England, kocha ambaye aliwahi kuifundisha Simba miaka ya nyuma ila walimfuta kazi baadae kwa kutoridhishwa na mwenendo wa timu.








8 months ago
Malunde10 Jun
ZIJUE MECHI 5 ZILIZOACHA ALAMA KOMBE LA DUNIA

Michezo ifuatayo ndiyo ilitoa matokeo ya kushangaza zaidi tangu kuanzishwa kwa mashindano ya kombe la Dunia kwa mujibu wa Gracenote.
5. Uruguay 2-1 Brazil 1950
Mchezo huu unashika nafasi ya tano ni kati Uruguay dhidi ya Brazil katika mashindano yaliyofanyika mwaka 1950 nchini Brazil. timu ya Uruguay ilishangaza wapenzi wa soka duniani baada ya kufanikiwa kuwafunga wenyeji 2-1Uruguay ilikuwa na asilimi 14.3 za uwezekano wa kushinda mechi hiyo huku Brazil ikihitaji alama moja kuweza kuwa mabingwa ilijikuta ikikabidhi ubingwa kwa Uruguay.
4. Ghana 2-0 Jamhuri ya Czech 2006
Ikiwa imepewa asilimia 13.9 za kushinda mechi Ghana, ilishangaza dunia kwa kuifunga Jamhuri ya Czech 2-0 katika kombe la dunia lililofanyika nchini Ujerumani mwaka 2006, matokeo hayo yaliwezesha timu ya Ghana kusonga mbele katika hatua ya 16 bora baada ya kushika nafasi ya pili katika kundi E nyuma ya Italy.
3. Algeria 2-1 Ujerumani Magharibi 1982
Kwa mujibu wa utafiti huo unaonesha kuwa mchezo huwa umeshika nafasi ya tatu katika matokeo ya kushangaza zaidi katika mashindano yaliyofanyika nchini Hispania. wakiwa katika kundi la pili, Algeria walikuwa na asilimia 13.1 tu ya kushinda lakini iliwafunga Ujerumani Magharibi 2-1.
2. Uswizi 1-0 Hispania 2010
Mashindano yaliyofanyika nchini Afrika Kusini, licha ya ubora wa kikosi cha Hispania lakini walijikuta wakipoteza mchezo dhidi ya Uswizi kwa kubali kipigo goli 1-0 katika mechi ya kwanza kundi G. Uswizi walikuwa na asilimia 10.3 za kushinda mechi hiyo.
1. Marekani 1-0 England 1950
Mchezo ulioshika nafasi ya kwanza ni mashindano ya kombe la Dunia yaliyofanyika nchini Brazil, Marekani iliifunga England goli 1-0 katika uwanja Belo Horizonte na Marekani ilikuwa na asilimia 9.5 za uwezekano wa kuifunga England kwa wakati huo.
8 months ago
BBCSwahili
Gor Mahia yaichapa Simba 2-0 mchezo wa fainali kombe la SportPesa
8 months ago
Michuzi
Waziri Mkuu atoa maelekezo kufufua michezo nchini
8 months ago
Zanzibar 2409 Jun
Raisi wa mchezo wa Kick Boxing Zanzibar ameitaka S M Z kuunga mkono mchezo huo
Raisi wa mchezo wa Kick Boxing Zanzibar ambaye amewahi kuwa Bingwa wa Mashindano mbali mbali Ashraf Suleiman ameitaka serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuunga mkono mchezo huo ambao utaitangaza Zanzibar kimataifa.
Akizugumza na Zanzibar24 nyumabani kwake Mpendae Ashraf amesema yeye binafsi ameteuliwa na Shirikisho la mchezo Kick Boxing duniani ( WKNY) kuwa Raisi wa Chama cha mchezo huo kwa upande wa Zanzibar ambao inapeperusha bendera kama Zanzibar.
Aidha Ashraf amefunguka na kusema kuwa yeye binafsi bado ameshakilia mataji mengi ambayo Mpaka leo hajapakonywa na mtu yeyote Mpaka leo na historia nayo duniani kama mzanzibari kwa miaka sita sasa.
“Tuliwahi kufika Baraza la Michezo Zanzibar mimi na raisi wa WKNY kunitambulisha kama mimi ndie Raisi baada ya kushinda mchezo wa dunia Kick Boxing” Alifahamisha Ashraf Sleman.
Kuhusu michezo ya kimataifa amefunguka na kusema tayari wameshapewa Mashindano ya kimataifa kama Zanzibar kusafiri nje ya nchi kwenye Mashindano mbali mbali kama vile ya Uingreza kwenda kugombania taji jengine mwezi saba tarehe 30.
“ Tarehe 28 mwezi ujao vijana wangu wanatarajia kwenda France kwenye kisiwa cha Mayole Mashindano yanayoitwa Kick Boxing Title mabondia kutoka Zanzibar watashiriki wanne Nassor Sindano kg 72, Bandago kg 77 na Viroba kg 79” Alifahamisha Ashraf Sleman.
Aidha Ashraf amewataka wadau kujitokeza kuunga mkono mchezo huo kwani ndio unaotangaza utalii wa Zanzibar hususan yeye anaposafiri kuwatangaza wazanzibari kwenye sekta ya utalii inakuwa na uchumi unakuwa kwa Zanzibar.
Jumla ya vijana 30 anawafundisha kwenye eneo lake la mazoezi kila siku ili kutengeza wanamichezo hao na kuukuza mchezo huo kwa ujumla ili jumla ya vijana nane tayari wameshafikia kiwango cha upiginaji kimataifa.
The post Raisi wa mchezo wa Kick Boxing Zanzibar ameitaka S M Z kuunga mkono mchezo huo appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Michuzi09 Jun
8 months ago
BBCSwahili
Chimbuko la mchezaji wa Man United na Ufaransa Paul Pogba
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Mchumba wa Diamond atambulisha gari lake aina ya BMW
Ikiwa ni takribani mwezi mmoja umepita tangu msanii Diamond Platnumz kukutana na mpenzi wake ambaye ni raia wa Kenya Tanasha Dona,
Tanasha ameamua kuitambulisha na kuionesha hadharani gari yake.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mwanadada, Tanasha ameioesha hadharani gari yake hiyo aina ya BMW yenye rangi ya blue.

Tanasha ameitambulisha gari hiyo na kuandika:-
Miss my BEAST baby blue
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Zahera afunguka makombe anayoyataka akiondoa Mapinduzi Cup
Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera ameweka wazi makombe ambayo ni vipaumbele kwake na klabu huku katika hayo akiondoa Mapinduzi Cup na ameeleza kuwa hatopeleka kikosi cha kwanza kwenye michuano hiyo.
Akiongea leo na wanahabari Zahera amesema kama klabu ni lazima wawe na vipaumbele na wakitaka kushiriki kikamilifu katika kila kombe basi watajikuta wanakosa yote hivyo kipaumbele chake ni ligi kuu na kombe la shirikisho.
“Kufuatana na nguvu yetu tulionayo kwa maana ya wachezaji, inatubidi...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Video: Madhara ya Kusherehekea Mwaka mpya 2019
Ikiwa Dunia inajiandaa kuupokea mwaka mpya 2019 ifikapo majira ya saa sita kamili za usiku wa leo, Waislamu kote nchini wametakiwa kuitumia siku hiyo kufikiri khatma ya maisha yao na si kusherehekea kama wanavyofanya wengine.
Kikawaida unapoingia mwaka mpya watu husherehekea kwa njia tofauti wengi wao hujichanganya katika kumbi za starehe baadhi hulewa na kuvunja chupa barabarani jambo ambalo limepingwa vikali kufanywa na waumini wa Dini ya kiislamu.
Kwa mujibu wa Naibu Katibu...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Dk: Shein asisitiza kudumishwa amani na utulivu visiwani Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewataka wananchi wa Zanzibar kuendelea kuidumisha hali ya amani na utulivu ambayo ndio msingi wa mafanikio yanayoendelea kupatikana hivi sasa na yatakayopatikana hapo baadae.
Dk. Shein ameyasema hayo leo katika risala yake ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2019 aliyoitoa kupitia vyombo vya habari, Ikulu mjini Zanzibar.
Dk. Shein amesema kuwa katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya mwaka 2018 mafanikio...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Naibu Katibu Mkuu mpya aahidi kusimamia kwa vitendo katiba ya CCM

NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Zanzibar Ndugu Othman Ally Maulid akizungumza mara baada ya kukabidhiwa Ofisi rasmi katika hafla iliyofanyika leo katika Afisi Kuu ya Wazazi Kikwajuni Unguja.
NAIBU Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Ndugu Othman Ally Maulid amesema atasimamia kwa vitendo ibara ya Tano ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 toleo jipya la mwaka 2017 inayoelekeza kuwa Ushindi wa CCM ni lazima kwa kila Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Chaguzi ndogo...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Magazeti ya Tanzania Leo Jumanne January 1, 2019
Kama kawaida Zanzibar24 tayari imeshakusogezea stori kubwa zilizotengeneza headline katika kurasa za mbele na nyuma za Magazeti ya Tanzania Leo Jumamosi January 1, 2019. Chukua time yako kwa kupitia Stori zote kali za udaku, siasa, michezo, burudani na mambo mengine mbali mbali.



















The post Magazeti ya Tanzania Leo Jumanne January 1, 2019 appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Fid Q amvisha pete ya uchumba mpezi wake
Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Fid Q amemvisha pete ya uchumba mpenzi wake.
Fid Q huyo ame-share picha kadhaa kwenye ukurasa wake wa Instagram zikionyesha hatua hiyo muhimu kuelekea kwenye maisha mapya ya ndoa.

Fid Q akiwa na mchumba wake
Itakumbukwa December 08 mwaka huu rapper kutoka kundi la Weusi, Nikki wa Pili naye pia alimvisha pete ya uchumba mpenzi wake.
The post Fid Q amvisha pete ya uchumba mpezi wake appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Wananchi wa kaskazini ‘A’ watakiwa kulitumia soko la Nungwi
Wananchi wa mkoa wa kaskazini Unguja wametakiwa kulitumia soko la wazi la kibiashara linalofunguliwa kila mwezi kwenye kijiji cha Nungwi ili kuweza kuuza na kununua biashara za asili zinazotengenezwa visiwani Zanzibar.
Akizungumza katika halfa ya ufunguzi wa soko hilo la kibiashara lililoandaliwa na tamwa Mkurugenzi wa halmashauri ya kaskazini A Mussa Ali Makame amesema kufunguliwa kwa soko la kuuza na kununua bidhaa mbalimbali za asili litaweza kutoa fursa kwa wananchi wakiwemo...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Bwana harusi afariki ghafla akisubiri kufunga ndoa
Sherehe ya harusi iliyokuwa ifanyike juzi jioni katika Kanisa la Nabii wa Utukufu wa Bwana lilipo Olmatejoo, Kata ya Sakina jijini Arusha na kwenye ukumbi wa Sariko Olasiti Garden, iligeuka msiba baada ya bwana harusi kufariki dunia ghafla akiwa kanisani.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 11 jioni katika kanisa hilo ambapo bwana harusi huyo, Heaven Makupa (47) alikuwa kanisani tangu saa saba mchana akisubiri kufunga ndoa na Jane Kimaro.
Hata hivyo, wakati sherehe, nderemo na vifijo...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Wenye mizani feki waingia matatani msako waaza
kuhakikisha kwamba mnunuzi wa bidhaa hapunjwi, Wakala wa Vipimo Nchini (WMA), wameendelea kufanya ukaguzi wa mizani zinazotumika sehemu tofauti hasa kwa wauzaji wa zao la korosho.
Lengo la kufanya hivyo ni kutaka kubaini mizani zisizo na viwango ambazo hazitoi kipimo kinachostahili.
WMA ilitembelea baadhi ya vyama vya msingi vya ushirika ili kushuhudia hali halisi ya upimaji korosho za wakulima.
Meneja wa WMA, mkoa wa Pwani, Evarist Masengo, alisema katika kuhakikisha wakulima...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
TRA yapigwa marufuku kufungia maduka na biashara
Serikali imeipiga marufuku Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kufunga maduka na biashara za watu kwa kisingizio cha kutolipa kodi.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango jana Desemba 30, 2018 wakati akitoa taarifa ya hali ya uchumi wa Taifa na utekelezaji wa bajeti ya Serikali katika nusu ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2018/19.
“Utaratibu wa kumfungia biashara mfanyabiashara anayedaiwa kodi ili kumshinikiza alipe sasa usitishwe mara moja, isipokuwa kwa wakwepa...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Yanga yawaacha Ajib na Makambo kombe la Mapinduzi
Kuelekea michuano ya kombe la Mapinduzi inayoanza kesho Januari 1, 2019 visiwani Zanzibar, klabu ya Yanga haitapeleka kikosi chake cha kwanza kwenye mashindano hayo.
Kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya Yanga kimeeleza kuwa baadhi ya wachezaji wa kikosi cha kwanza wamepewa mapumziko na kocha Mwinyi Zahera ili kujiweka sawa kwaajili ya mechi za ligi kuu.
”Badala ya kwenda na kikosi cha kwanza mwalimu ameeleza kuwa Yanga itakwenda na wachezaji ambao wamekuwa hawapati nafasi ili nao waweze...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Manara awashtaki Yanga Mamlaka ya mapato’TRA’
Msemaji wa Klabu ya Simba, ambao pia ni Mabingwa Watetezi, Haji Manara amehoji Mamlaka ya mapato Tanzania juu utaratibu wa watani zao wa jadi kuhusu kuchangisha kwa ajili ya klabu yao na kuuliza kama utaratibu huo ni sahihi.
Manara amehoji iwapo kama Klabu hiyo inayoongoza msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara kama inalipia kodi katika Mamlaka hiyo huku akisistiza kwamba hata kama ukweli ukiwa mchungu kiasi gani lazima usemwe.
“TRA nakumbuka mlienda katika kanisa la Mchungaji...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Afariki akiwa mapajani mwa mwanamke
Mwanaume mmoja katika kijiji cha Gionsaria,kaunti ya Kisii Nchini Kenya amefariki dunia baada ya mwanamke mmoja kumbana /kufungia kichwa cha mwanaume huyo katikati ya mapaja.
Tukio hilo limetokea siku ya Ijumaa Disemba 28,2018, Chifu wa eneo hilo Oganda Matego amesema mwanaume huyo anayejulikana sana kwa jina ‘Doctor’,ambaye pia ni taniboi wa magari ya kusafirisha majani ya chai eneo hilo, alibanwa kichwa chake katikati ya mapaja/miguu na mwanamke mmoja.
Amesema wakati mwanamke huyo...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
PAZA yabadilisha maisha ya Wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja
Mradi wa kukuza uwajibikaji Zanzibar (PAZA) ulioundaliwa na TAMWA kwa kushirikiana na WAHAMAZA na NGENARECO pamoja na Asasi za kiraia waibua maendeleo ya kimaisha kwa Wananchi wa Kaskazini Unguja.
Akizungumza na Zanzibar24 blog Katibu wa Jumuia ya vijana kupambana na udhalilishaji Ali Makame Zuberi huko Gamba Wilayani Mkoa wa Kaskazini Unguja amesema katika mradi huo wamepata mafanikio makubwa ambayo kwakiasi fulani ipelekea jamii kuhamasika kwa njia tofauti za kimaisha.
Amesema...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
OmbaOmba: Janga linalokua kwa kasi kijiji cha Nungwi
Wamiliki wa mahotel kijiji cha Nungwi wamewataka wazazi na walezi wanaoishi karibu na mahoteli kuwazuia watoto na kuwakataza tabia ya kuomba omba watalii kwani hatua hiyo itaweza kuwasababishia kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji.
Wakizungumza kwa masikitiko makubwa baadhi ya wamiliki wa mahoteli hao ambao wamekataa kutajwa majina yao wamesema tabia ya kuomba omb pia ni chanzo cha udhalilishaji kwa watoto kwani wapo baadhi ya wageni hawatoi pesa zao bure.
Wamesema wazazi...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
TANGAZO LA UHAKIKI WA WASTAAFU ZSSF
MFUKO WA HIFADHI YA JAMII ZANZIBAR (ZSSF) UNAWATANGAZIA WASTAAFU WANAOPOKELEA PENCHENI YA ZSSF KUPITIA BENKI TOFAUTI KUWA UHAKIKI KWA WANACHAMA SASA UTAFANYIKA MWANZONI MWA MWEZI WA JANUARI 2019
KWA WASTAAFU WOTE WA UNGUJA NA PEMBA UHAKIKI HUO UTAFANYIKA KUANZIA TAREHE 02 HADI 11 JANUARI 2019 KUANZIA SAA 2:00 ZA ASUBUHI
UHAKIKI HUO UTAFANYIKA KATIKA AFISI ZA ZSSF KILIMANI MNARA WA MBAO NA TIBIRINZI CHAKECHAKE PEMBA.
AIDHA KWA WASTAAFU WALIOPO DAR ES SALAAM UHAKIKI WAO UTAFANYIKA...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
11 wagunduliwa na Saratani ya Shingo ya Kizazi Zanzibar
Jumla ya Wanawake 11 kati ya 3013 waliopimwa Saratani ya Shingo ya kizazi, awamu ya kwanza, wamegundulika kuwa na maradhi hayo na wengine 48 wameonyesha kuwa na dalili na hatua za kuwapatia matibabu zilianza baada ya kugunduliwa.
Waziri wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed alieleza hayo katika hafla ya kuwaaga na kuwapongeza Madaktari wa kichina, kutoka Jimbo la Jiangsu, baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya Mradi wa uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya kizazi ulioanza tarehe 03 na...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Seleman Matola apata jeuri baada ya kutoka sare na Simba
Seleman Matola ambaye ni Kocha wa Lipuli FC, amesema kuwa jeuri ya kikosi chake kuwa na mwendelezo wa kupata matokeo mazuri ni sare waliyoipata na Simba kwenye mchezo wa Ligi Kuu waliocheza uwanja wa Taifa.
Baada ya sare hiyo, Lipuli walifanikiwa kukusanya pointi 9 katika michezo ya Ligi kuu waliyocheza ambayo ni pamoja na Mbeya City kwa kuwachapa bao 2-0 wakiwa ugenini, walishinda pia dhidi ya Ruvu Shooting uwanja wa Samora, Biashara United Samora na kesho watakuwa nyumbani dhidi ya...
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Shirika la Umeme laomba radhi latoa sababu iliyopelekea kukatika kwa umeme
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), limeomba radhi wateja wake wa mikoa iliyounganishwa na gridi ya Taifa kwa katizo la umeme lililotokea leo Desemba 29, 2018 majira ya Saa 9:00 Alfajiri.
Kupitia ukurasa wa mtandao wa kijamii wa Twitter, TANESCO imesema kwamba sababu iliyopelekea kukatika kwa umeme ni hitilafu iliyotokea katika mfumo wa gridi.
Hata hivyo taarifa hiyo imesema kwamba wataalamu na mafundi wa shirika hilo wanaendelea na jitihada za kuhakikisha umeme unarejea kwa haraka...
Eatv.Tv
Leo Februari 16, msanii Godzilla anatarajia kuzikwa kwenye makaburi ya Kinondoni saa 10 Jioni....
Leo Februari 16, msanii Godzilla anatarajia kuzikwa kwenye makaburi ya Kinondoni saa 10 Jioni. RATIBA IKO KAMA IFUATAVYO: Mwili utawasili nyumbani saa 3 asubuhi Chakula saa 4 asubuhi Kuelekea kanisani saa ibada saa 5:30 Ibada itaanza saa 6:00 mchana. Kuelekea uwanjani Salasala saa 7:00 Mchana kutoa heshima za mwisho, baada ya hapo wataelekea Kinondoni makaburini kwa ajili ya mazishi. R. I. P Golden Jacob Mbunda (Godzilla/King Zilla)
Ladyjaydee
Mkandamizaji
Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua...
Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe. Kufa ni faida na kuishi ni Kristo. Pumzika kwa amani Jacob.
FidHop
MAFANIKIO hayaji ukikata TAMAA/ yenyewe huwafuata wanaojituma na wale wasiosukumwa na NJAA... 📌
MAFANIKIO hayaji ukikata TAMAA/ yenyewe huwafuata wanaojituma na wale wasiosukumwa na NJAA... 📌
2 months ago
MichuziSERIKALI YAPOKEA GAWIO LA SH. BILIONI 10.1 KUTOKA NMB
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
2 months ago
MichuziPROF. KAMUZORA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CHINA NCHINI TANZANIA

2 months ago
BBC
Zeinab Mohammed Salih: Fashion police shave off afros
2 months ago
BBCSwahili
Msako mkali dhidi ya makanisa ya kikristo umeanza China na kuzua taharuki
8 months ago
MichuziVODACOM TANZANIA YAFUTURISHA WATEJA WAKE JIJINI DAR
Baadhi ya wateja na wafanyakazi wa mtandao wa simu wa Vodacom Tanzania wakichukua futari, wakati wa hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na mtandao huo jijini Dar es Salaam
8 months ago
MichuziTPA TANGA YAIBUKA MSHINDI KWA TAASISI ZA KISERIKALI ZILIZOSHIRIKI MAONESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA JIJINI TANGA
8 months ago
MichuziAirtel kuendelea kuboresha huduma zake kwenda na teknolojia
Kampuni ya simu za mkononi Airtel Tanzania imehaidi kuendelea kutoa huduma bora na za kisasa kwa wateja wake. Hii ni kutatua kero na changamoto ambazo zimekuwa zikiikumba sekta ya mawasiliano hapa nchini.
Akiongea jijini Dar es Salaam jioni baada ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa wateja na washirika wake, Mkurugenzi wa Biashara kwa wateja maalum Airtel Tanzania Boniface Bwambo alisema kampuni hiyo itaendelea kutoa huduma bora na za kisasa ili kukidhi matakwa ya wateja wake pamoja na kuongeza pato kutoka na huduma zake kwenye kipindi hiki ambacho ushindani umekuwa mkubwa kwenye sekta ya mawasiliano.
Bwambo alisema baadhi ya bidhaa mpya zinazotolewa na kampuni hiyo ili kwenda na wakati ni fixed portfolio ambayo huwapa wateja nafasi ya kufurahia huduma ya mtandao ya kasi ya Fiber Solutions, Line Solutions na Co-Location Solutions. Huduma hizi ni suluhisho kwa biashara za mtandaoni, inapatikana kwa gharama nafuu katika vifurushi zinazotolewa na Airtel.
Bwambo alisema hayo wakati wa futari iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam. ‘Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kipindi muhimu sana kwa waumini wa dini ya Kislam duniani kote. Kwa kutambua umuhimu huo, sisi Airtel tumeona ni Faraja kukutana hapa siku ya leo na kufuturu kwa pamoja. Hii ni moja ya njia nzuri pia kukutana na wateja na kuonyesha tunawajali. Vile vile, kwa kukutana pamoja hapa inatoa fursa ya kuzungumza na kuonyesha baadhi ya bidhaa zetu kwa wateja wetu, aliongeza Bwambo.
‘Ni furaha sana kuwa nasi zote hapa. Ni furaha zaidi kuweza kutambua kuwa sisi Airtel tunatoa huduma zaidi ya mawasiliano. Kwa kuongea tu ni kwamba wengi wanajua huduma yetu ya Airtel Money ni kutuma na kupokea fedha na kununua au kulipia bidhaa. Lakini vile vile imeenda zaidi kwa kuweza kukusanya mauzo au mapato kwa wateja na kupeleka moja kwa moja kwenye akaunti yake ya benki. Kwa sasa mfanya biashara hana haja ya kutoka kukusanya mauzo ua mapato kwa sisi kupitia Airtel Money tufanya kazi hio na ndio sababu tunasema Airtel Money ni salama na njia nafuu ya kuweka na kutunza fedha. Alisema Bwambo .
Kwenye tukio la futari hiyo alikuwepo pia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Tanzania Sanjay Rughani. Alipongeza kampuni ya Airtel kwa kutambua umuhimu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na pia kwa kutoa huduma bora na nafuu kwa wateja wake.
‘Airtel inafanya vizuri kwa kuboresha huduma zake kila siku ili kwenda na wakati kitu ambacho ni muhimu kwa wateja na washirika wake kama sisi. Kuja kwangu hapa leo kumeweza kunipa na kutambua huduma na bidhaa mpya kutoka Airtel ambazo nilikuwa sina taarifa nazo hapa awali. Hii ni jambo la kupongezwa sana, alisema Rughani.
On her side the Administration and Project Manager of the National Industrial and Commercial (NIC) Bank, MsBadriaLema, said out of enjoying sharing iftar with the Airtel staffs and other people, she gets a chance to know other services offered by the company especially Airtel Money profit distribution.
Kwa upande, Meneja Utawala na miradi wa benki ya NIC Tanzania Badrial Lema alisema ni furaha kubwa kuungana na wafanya kazi wa Airtel Tanzania kushiriki futari ya leo. ‘Nimefurahi sana kukutana na wafanyakazi wa Airtel na wageni wengine waalikwa. Ni tukio la iana yake kwani nimeweza kupata marafiki wapya na kuongeza ufahamu juu ya huduma zinazotolewa na Kampuni ya Airtel Tanzania.
8 months ago
Zanzibar 2408 Jun
Airtel yatangaza huduma mpya yajipanga kuboresha huduma zake
Kampuni ya simu za mkononi Airtel Tanzania imehaidi kuendelea kutoa huduma bora na za kisasa kwa wateja wake. Hii ni kutatua kero na changamoto ambazo zimekuwa zikiikumba sekta ya mawasiliano hapa nchini.
Akiongea jijini Dar es Salaam jana jioni baada ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa wateja na washirika wake, Mkurugenzi wa Biashara kwa wateja maalum Airtel Tanzania Boniface Bwambo alisema kampuni hiyo itaendelea kutoa huduma bora na za kisasa ili kukidhi matakwa ya wateja wake pamoja na kuongeza pato kutoka na huduma zake kwenye kipindi hiki ambacho ushindani umekuwa mkubwa kwenye sekta ya mawasiliano.
Bwambo alisema baadhi ya bidhaa mpya zinazotolewa na kampuni hiyo ili kwenda na wakati ni fixed portfolio ambayo huwapa wateja nafasi ya kufurahia huduma ya mtandao ya kasi ya Fiber Solutions, Line Solutions na Co-Location Solutions. Huduma hizi ni suluhisho kwa biashara za mtandaoni, inapatikana kwa gharama nafuu katika vifurushi zinazotolewa na Airtel.
Bwambo alisema hayo wakati wa futari iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam. ‘Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kipindi muhimu sana kwa waumini wa dini ya Kislam duniani kote. Kwa kutambua umuhimu huo, sisi Airtel tumeona ni Faraja kukutana hapa siku ya leo na kufuturu kwa pamoja. Hii ni moja ya njia nzuri pia kukutana na wateja na kuonyesha tunawajali. Vile vile, kwa kukutana pamoja hapa inatoa fursa ya kuzungumza na kuonyesha baadhi ya bidhaa zetu kwa wateja wetu, aliongeza Bwambo.
‘Ni furaha sana kuwa nasi zote hapa. Ni furaha zaidi kuweza kutambua kuwa sisi Airtel tunatoa huduma zaidi ya mawasiliano. Kwa kuongea tu ni kwamba wengi wanajua huduma yetu ya Airtel Money ni kutuma na kupokea fedha na kununua au kulipia bidhaa. Lakini vile vile imeenda zaidi kwa kuweza kukusanya mauzo au mapato kwa wateja na kupeleka moja kwa moja kwenye akaunti yake ya benki. Kwa sasa mfanya biashara hana haja ya kutoka kukusanya mauzo ua mapato kwa sisi kupitia Airtel Money tufanya kazi hio na ndio sababu tunasema Airtel Money ni salama na njia nafuu ya kuweka na kutunza fedha. Alisema Bwambo .
Kwenye tukio la futari hiyo alikuwepo pia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Tanzania Sanjay Rughani. Alipongeza kampuni ya Airtel kwa kutambua umuhimu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na pia kwa kutoa huduma bora na nafuu kwa wateja wake.
‘Airtel inafanya vizuri kwa kuboresha huduma zake kila siku ili kwenda na wakati kitu ambacho ni muhimu kwa wateja na washirika wake kama sisi. Kuja kwangu hapa leo kumeweza kunipa na kutambua huduma na bidhaa mpya kutoka Airtel ambazo nilikuwa sina taarifa nazo hapa awali. Hii ni jambo la kupongezwa sana, alisema Rughani.
On her side the Administration and Project Manager of the National Industrial and Commercial (NIC) Bank, MsBadriaLema, said out of enjoying sharing iftar with the Airtel staffs and other people, she gets a chance to know other services offered by the company especially Airtel Money profit distribution.
Kwa upande, Meneja Utawala na miradi wa benki ya NIC Tanzania Badrial Lema alisema ni furaha kubwa kuungana na wafanya kazi wa Airtel Tanzania kushiriki futari ya leo. ‘Nimefurahi sana kukutana na wafanyakazi wa Airtel na wageni wengine waalikwa. Ni tukio la iana yake kwani nimeweza kupata marafiki wapya na kuongeza ufahamu juu ya huduma zinazotolewa na Kampuni ya Airtel Tanzania.
The post Airtel yatangaza huduma mpya yajipanga kuboresha huduma zake appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Zanzibar 2408 Jun
Mkurugenzi wa Benki ya KCB awatoa hofu wateja wake
Mkurugenzi mtendaji wa Benki ya biashara ya Kenya KCB Cosmas Kimario amewatoa hofu wananchi na hasa wateja wa benki hiyo juu ya amana zao walizoeka kuwa ni salama kutokana na kuwa na Mtaji wa kutosha katika kuendeshea huduma za kifedha.
Akizungumza na zanzibar24 mara baada ya futari iliyoandaliwa na Benki hiyo kwa watendaji wake iliyofanyika Mjini Zanzibar Kimario amesema katika sekta ya fedha kwa benki hiyo iko vizuri kutokana na kuwa na msimamizi mzuri ambae ni Benki kuu ya Tanzania BOT na inataarifa zote za uendeshaji wa benki hiyo.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo amesema licha ya kuwa na mafanikio katika uendeshaji wa huduma za kibenki pia wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ikiwemo baadhi ya wateja kutorudisha mikopo kwa wakati na kusababisha usumbufu katika huduma hiyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Huduma za KCB Sahl Benki Rashid Rashid amewahimiza wananchi kuweka amana zao kupitia Sahl benki ambayo inafuata misingi ya ShEria ya dini ya kiislam na utendaji kazi wake hufuata maendeleo ya kiuchumi ya kiislam.
Nae Mjumbe wa bodi ya sharia elekezi wa Benki hiyo ya KCB Sheikh Twaha Bane amewataka wananchi mbali mbali kufukuzia fursa zinazotolewa na Benki hiyo kupitia huduma zinazotolewa kwa mfumo wa kiislam ili kujiepusha na riba ambayo anaichukia Mwenyezi Mungu.
Fat-hiya Shehe
The post Mkurugenzi wa Benki ya KCB awatoa hofu wateja wake appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Michuzi
Benki ya CRDB na Jeshi la Polisi nchini kudumisha mahusiano ya kibiashara



8 months ago
Reuters Africa07 Jun
Maasai clash with Tanzania in court over eviction from Serengeti
Business Daily
Reuters Africa
NAIROBI, June 7 (Thomson Reuters Foundation) - Maasai herders near Tanzania's famous Serengeti wildlife park have asked a regional court to stop the government intimidating witnesses supporting their legal bid to return to their ancestral land, a ...
Mara hotels fully booked ahead of wildebeest migrationBusiness Daily (press release) (blog)
all 2 news articles »
8 months ago
Michuzi
Kampuni ya Auxin ya China yaonesha nia kuwekeza kwenye kiwanda cha Baruti





8 months ago
Zanzibar 2407 Jun
Vigogo wa Halotel na Zantel wasekwa rumande
The post Vigogo wa Halotel na Zantel wasekwa rumande appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Malunde
VIGOGO WA HALOTEL NA ZANTEL WATUPWA MAHABUSU

Makosa yao yanahusisha kula njama, kuingiza, kufunga mitambo, matumizi ya laini za simu bila usajili wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh. bilioni moja.
Washtakiwa hao walisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Mfawidhi, Calvin Mhina, anayesikiliza usikilizwaji wa awali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga akisaidiana na Wakili wa Serikali, Jaqline Nyantori.
Nyantori aliwataja washtakiwa wengine ni Lei Cao maarufu kama Peter (28), Huang Yu Meng (27), Msimamizi wa Biashara wa Halotel Zanzibar, Jimmy Mosha (26), Meneja Masoko Halotel, Willy Ndoni (29), Kampuni ya Viettel Tanzania Ltd maarufu kama Halotel iliyopo Kinondoni, na Kampuni ya ZanzibarTelecomunication PLC maarufu kama Zantel ilioyopo Msasani, jijini Dar es Salaam.
Alidai katika shtaka la kwanza, kati ya Januari Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu nchini Tanzania, mshtakiwa wa kwanza hadi wa sita, walikula njama ya kutenda kosa la kutumia huduma za mawasiliano kwa njia ya udanganyifu.
Shtaka la pili, katika ya Mei Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu katika jengo la Spring lililopo Mbezi, mshtakiwa wa kwanza hadi wa sita, kwa pamoja walifunga mitambo ya mawasiliano kwa njia ya udanganyifu na kujipatia huduma za mtandao wa Halotel na Zantel bila kibali cha TCRA .
Shtaka la tatu, nne, tano na sita kati ya Januari Mosi na Desemba 31, 2017, Aprili 30,mwaka huu jijini Dar es Salaam, mshtakiwa wa tatu na wa nne, waliingiza nchini, waliifunga na kuendesha mitambo ya mawasiliano kwa kuunganisha na kampuni hizo za simu bila kibali cha TCRA.
Shtaka la nane, kati ya Mei Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu katika jengo la Spring City, mshtakiwa wa tatu na wanne, walikutwa wakitumia laini za simu za mkononi zisizosajiliwa na TCRA 281,272 za Halotel na 11,920 za Zantel.
Aidha, upande wa Jamhuri ulidai katika shtaka la 10 kati ya Mei, 2017 na Aprili 30, mwaka huu katika matawi ya Zantel ya jijini Dar es Salaam, mshtakiwa wa pili na wa nane walitumia kwa makusudi laini za simu 11,920 zisizokuwa na usajiliwa TCRA.
Shtaka la 11 na 12, kati ya Mei Mosi, 2017 na Aprili 30, mwaka huu, washtakiwa waliisababishia serikali hasara ya Sh. 1,131,936,400.
Kwa mujibu wa mashtaka yanayowakabili washtakiwa, kisheria hawakutakiwa kujibu chochote hadi upelelezi utakapokamilika itasilizwa Mahakama Kuu Tanzania, Divisheni ya Uhujumu Uchumi au kwa kibali maalumu kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).
Hakimu Mhina alisema kesi hiyo itatajwa Juni 20, mwaka huu na washtakiwa watakwenda mahabusu.
8 months ago
Michuzi
WAJUMBE KAMATI ZA BAJETI NA UONGOZI WASHAURIANA NA SERIKALI KUHUSU HOJA ZENYE MASLAHI KWA TAIFA

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti na Mbunge wa Mtwara Vijijini, Mhe. Hawa Ghasia akizungumza wakati wa Mashauriano kati ya kamati ya Bajeti, kamati ya Uongozi na Serikali kuhusu Hoja zenye Maslahi kwa Taifa zilizojitokeza wakati wa Bajeti za Wizara kwa Mwaka 2017/2018 na Makadirio ya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 yaliyofanyika leo katika Ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Bajeti na Mbunge wa Babati Vijijini Mhe. Jitu Soni




(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
8 months ago
MichuziPROF. MBARAWA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA USIKU KAMBI YA SOGA YA UJENZI WA RELI YA MWENDOKASI ‘SGR’…ATOA MAAGIZI MAZITO
Na John Nditi, Kibaha
WAZIRI wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano , Profesa Makame Mbarawa ameitaka Kampuni ya Yapi Merkezi ya nchini Uturuki inayojenga reli ya kisasa (Standard Gauge)’SGR’ kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro urefu wa kilomita 300 kuongeza kasi na kufanya kazi mchana na usiku ili ujenzi huo ukamikike kwa wakati kulingana na makubaliano ya kimkataba.
Profesa Mbarawa alitoa kauli hiyo alipofanya ziara ya kushitukiza Juni 5, mwaka huu ( 2018) majira ya saa tano siku kwenye kambi ya Reli ya Mwendokasi iliyopo Soga , wilayani Kibaha mkoani Pwani na kuendesha ukaguzi hadi saa sita usiku maeneo mbalimbali ya ujenzi wa njia ya SGR.
Alisema , lengo la kufanya ziara ya kushitukiza ni kujionea namna walivyojipata kuhakikisha kazi zinafanyika saa 24 mchana na usiku ndani ya siku saba za juma.
Profesa Mbarawa alisema , lengo ni kuona makubaliano kati ya mkandarasi na Serikali ya kukamilishwa kwa ujenzi huo ifikapo Novemba mwaka 2019 unatimizwa na wananchi kunufaika na mradi huo mkubwa.
Hata hivyo , Waziri aliwakuta wafanyakazi na wahandisi wa mradi huo wa kiwa maeneo yao ya kazi , ambapo aliwataka watanzania walipata fursa ya kusimamia kazi hiyo kuwepo eneo la mradi kipindi chote cha saa 24 na kupangiana zamu za kazi .
Alisema , hatua hiyo itawezesha shughuli ya ujenzi iendelee kwa kasi zaidi na kwa muda wote kama ilivyopangwa ndani yamakubaliano na kazi hiyo inafanyika kwa viwango vya ubora na ufanisi mkubwa.
Pamoja na hayo alitumia fursa hiyo kumkata mkandarasi wa ujenzi huo kupitia Meneja mradi , Kemal Artuz kuogeza kasi ya ujenzi ili kufikiwa makubaliano ya kukamilishwa kwa ujenzi wa reli hiyo kwa wakati kuwezesha watanzania kunufaika na matunda hayo.
“ Tayari wameanza kujenga tuta na sehemu nyingine wameweka kokoto kabla ya kuweka mataaluma , kazi inaenda vizuri “ alisema Profesa Mbarawa na kuongeza .
“ Tuta linalojengwa linapaswa liwe na vipimo na viwango vilivyokubalika kwa pamoja kimkataba ili reli hii ya kisasa inayotumia umeme itakuwa na uwezo wa kusafiri kwa mwendokasi wa kilomita 160 kwa saa kwa treni ya abiria ” alisema Profesa Mbarawa.
Waziri alisema , treni ya mizigo itakuwa na uwezo wa kusafiri kwa kilometa 120 kwa saa na kubeba mizigo tani 10,000 kwa wakati mmoja na kwa maana hiyo itaweza kuondoa barabarani mizigo tani 20 kwa magari 500 wakati mmoja. Profesa Mbarawa alitaja kipande cha reli kingine kitakachojengwa ni kutoka Morogoro- Makutupola chenye urefu kilometa 422 .
Waziri Mbarawa alisema ,reli ya kwendo kasi itakayokuwa imejengwa kutoka Dar es Salaam hadi Makutupola itakuwa na urefu wa kilometa 722 na ujenzi wake utagharimu kiasi cha Sh trrioni 7.06.7 fedha zinagharamiwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Tanzania.
“ Kazi niafanyika mchana na usiku kama mlivyotukuta na mheshimiwa Waziri … na inafanyika kwa ubora na umakini na sasa tumefikia kwa baadhi ya maeneo kumwaga kokoto na baada kuweka mataaluma “ alisema Mhandisi Rutaihwa.
8 months ago
Malunde06 Jun
MTUNGI WA GESI WATEKETEZA NYUMBA DODOMA

Moto mkubwa unaosemekana umesababishwa na kulipuka kwa jiko la nishati ya gesi umeteketeza nyumba moja yenye vyumba sita iliyopo katika mtaa wa hazina x jijini Dodoma na kuharibu mali za baadhi ya wapangaji waliokuwa wakiishi ndani ya nyumba hiyo.
Wakizungumza na waandishi wa habari baadhi ya wapangaji wa nyumba hiyo Maimuna Hussein na Nickson Steven wamesema moto huo umetokea saa 3:40 asubuhi na kuteketeza baadhi ya mali zao.
Kwa upande wake Mkuu wa kikosi cha zimamoto na uokoji mkoa wa Dodoma, kamishna msaidizi Regina Kaombwe, amesema baada ya kupata taarifa ya kuungua kwa nyumba hiyo waliwahi eneo la tukio na kisha ametoa wito kwa wakazi wa jiji hilo.
8 months ago
Michuzi
KIGWANGALLA AAGIZA MSAKO MKALI KWA WALIOUA SIMBA TISA SERENGETI
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameagiza Kikosi Kazi Dhidi ya Ujangili cha Taifa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Serengeti kuwasaka watu waliohusika na mauaji ya simba tisa katika kijiji cha Nyichoka, wilaya ya Serengeti mkoani Mara na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
Dkt. Kigwangalla ametoa agizo hilo ofisini kwake Jijini Dodoma jana baada ya kupokea taarifa rasmi ya mauaji hayo ya kikatili yaliyoripotiwa hivi karibuni kwa simba hao kulishwa sumu kali katika kijiji hicho huku mmoja akikatwa miguu, mkia, ngozi ya juu ya mgongo na kuchukuliwa baadhi ya viungo vyake ambapo amesema mauaji hayo hayavumiliki kwa kuwa yana athari kubwa kiikolojia, kiutalii na uchumi wa Taifa kwa ujumla.
"Bahati mbaya sana ni kuwa anapouawa simba kwa sumu hafi peke yake, inakufa familia nzima ya simba, na mara nyingi wanakufa pia wanyamapori wengine wanaodowea nyama na wanaokula mizoga. Walipouawa simba wa Ruaha hivi karibuni walikufa fisi zaidi ya 70 na ndege mbeshi zaidi ya 100, achilia mbali wadudu," amesema Dkt. Kigwangalla kwa masikitiko makubwa.
Amesema pamoja na faida kubwa za simba kwa Taifa kiuchumi, Kijiji cha Nyichoka pekee walikouwawa simba hao ni katika sehemu iliyofaidika sana na miradi ya ujirani mwema kutoka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti."Wanyama hawa jamii ya paka wakubwa ni muhimu sana kwa kuweka mizania ya ikolojia sawa, maana wanadhibiti idadi ya wanyama wala nyasi kwa kuwala, bila hivyo hifadhi zote zinaweza kugeuka kuwa jangwa.



HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
8 months ago
Michuzi
RC MGHWIRA ATOA ONYO KALI KWA WANAOHARIBU MIUNDOMBINU YA TANESCO
Mkuu huyo wa mkoa alisema, serikali inatumia gharama kubwa sana kuendesha shirika hilo hivyo kulihujumu kwa kuharibu miundimbinu sio sahihi na halivumiliki.
Aliyasema hayo jana wakati akiongea na waandisi wa habari, katika kampeni maalumu inayofanywa na Tanesco makao makuu ikiwa na lengo la kuhamasisha juu ya athari za kuhujumu miumbombinu ya shirika hilo.
“Hivi karibuni kumekuwepo na matukio ya baadhi ya watu kupoteza maisha baada ya kujaribu kujiunganishia umeme kwa njia ya wizi. naagiza wakazi wa mkoa huu kuacha kabisa tabia hiyo kwani matukio ya aina hiyo ni sawa na matukio ya uhujumu uchumi, ambayo yanarudisha nyuma jitihada za Serikali za kuhakikisha nishati ya umeme inapatikana na hivyo kufikia uchumi wa kati kupita viwanda,” alisema
Aliongeza kuwa uhujumu wa miundombinu sio tu inaleta hasara kwa shirika lakini pia inapelekea kupoteza nguvu kazi ya taifa kupitia maafa mbalimbali ikiwemo vifo na ulemavu kwa watu wanaohusika na matukio hayo. Naye Meneja wa Tanesco Mkoa wa Kilimanjaro Mahawa Mkaka alisema changamoto ya uharibifiu wa miumbombinu unatokana na uelewa mdogo kuhusiana na madhara yatokanayo na umeme.






KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
8 months ago
AllAfrica.Com05 Jun
Tanzania: You've Failed Farmers in a Big Way, Magufuli Tells Bank
AllAfrica.com
Dar es Salaam — President John Magufuli yesterday expressed his displeasure at the Tanzania Agricultural Development Bank's failure to empower farmers despite over Sh360 billion having been injected into bank for the purpose. President Magufuli also ...
and more »
2 months ago
Zanzibar 2401 Jan
Mchumba wa Diamond atambulisha gari lake aina ya BMW
Ikiwa ni takribani mwezi mmoja umepita tangu msanii Diamond Platnumz kukutana na mpenzi wake ambaye ni raia wa Kenya Tanasha Dona,
Tanasha ameamua kuitambulisha na kuionesha hadharani gari yake.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram mwanadada, Tanasha ameioesha hadharani gari yake hiyo aina ya BMW yenye rangi ya blue.

Tanasha ameitambulisha gari hiyo na kuandika:-
Miss my BEAST baby blue @bmw” lakini chini ya post hiyo msanii Diamond ambaye ndio mpenzi wake amecomment chini na kuweka viemoj vya moto


Ingawa kwenye post hiyo watu wengi wakiweka comment zao na kudai kuwa amehongwa na Diamond.
The post Mchumba wa Diamond atambulisha gari lake aina ya BMW appeared first on Zanzibar24.
2 months ago
MwanaHALISI01 Jan
Mwalimu aliyemfungia mtoto kabatini azidi kubanwa
2 months ago
RFI
Wanyarandwa waomboleza kifo cha Shujaa wa mauaji ya kimbari
2 months ago
Malunde
POLISI DODOMA WAKANUSHA MTOTO WA MTOTO KUFUNGIWA KABATINI

Binti huyo wa miaka 15, jana Desemba 30, 2018 akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma alidai kufanyiwa ukatili kwa kupigwa na kufanyishwa kazi hadi usiku wa manane na bosi wake anayedaiwa kuwa ni mwalimu na kwamba amekuwa akimwambia amfungie hadi usiku mtoto wake na kila alipovunja masharti alikumbana na kipigo.
Leo Desemba 31, 2018 polisi mkoani Dodoma imekanusha madai ya mtoto huyo kufungiwa kabatini kama inavyodaiwa, lakini wamekiri binti huyo kushambuliwa na mwajiri wake.
Kamanda wa polisi mkoani humo, Gilles Muroto amesema polisi wamefanya upekuzi katika nyumba ya mwajiri wa binti huyo ambaye kitaaluma ni mwalimu, Anitha Kimako na kubaini hakuwa na kabati nyumbani kwake.
"Kesi ya shambulio ipo na ameshambuliwa kweli na ndiyo maana tunamshikilia. Anashikiliwa kutokana na usalama wake kwani kelele za watu ni nyingi, ila hili suala la kuwekwa mtoto kabatini halipo," amesema Muroto.
Amesema uchunguzi wa kina unafanyika na kwamba lazima mwalimu huyo wa Shule ya Msingi Medali afikishwe mahakamani.
2 months ago
Malunde
MWANAUME AFARIKI KATIKATI YA MAPAJA YA MWANAMKE

Mwanaume mmoja katika kijiji cha Gionsaria,kaunti ya Kisii Nchini Kenya amefariki dunia baada ya mwanamke mmoja kumbana /kufungia kichwa cha mwanaume huyo katikati ya mapaja.
Mkasa huo wa aina yake umetokea siku ya Ijumaa Disemba 28,2018.
Chifu wa eneo hilo Oganda Matego amesema mwanaume huyo anayejulikana sana kwa jina ‘Doctor’,ambaye pia ni taniboi wa magari ya kusafirisha majani chai eneo hilo, alibanwa kichwa chake katikati ya mapaja/miguu na mwanamke mmoja.
Amesema wakati mwanamke huyo akiwa amebana kichwa cha mwanaume katikati ya mapaja, rafiki wa mwanamke huyo ambaye pia ni mwanamke alikuwa ameshikilia miguu ya ‘Doctor’na kumuinua hewani/juu.
Oganda amesema inashukiwa kuwa wawili hao walikuwa wapenzi na kifo cha ‘Doctor’ kilitokea wakicheza ambapo baada ya dakika moja mwanaume aliachilia kichwa na kubamiza kichwa kwenye barabara ya lami.
Inaelezwa kuwa wanawake hao walimpeleka ‘Doctor’ katika hospitali ya wilaya ya Nyamache na madaktari walipompima wakabaini kuwa tayari alikuwa amefariki dunia.
Tayari wanawake hao wanashikiliwa na polisi kwenye kituo cha polisi cha Nyangusu huku wakisubiri kufunguliwa mashtaka.
Aidha baada ya habari ya kifo cha ‘Doctor’ kuwafikia majirani wa wanawake hao,waliamua kuchoma nyumba nne zinazomilikiwa na hao wanawake.
Hali ya utulivu imeshuhudiwa kwa sasa na Chifu wa eneo hilo Oganda Matego amewasihi wakazi wa eneo hilo kutochukua sheria mikononi mwao kiholela.
SOMA ZAIDI HAPA
2 months ago
Malunde
MABAKI YA MWILI WA MSTAAFU ALIYEPOTEA BAADA KUPOKEA MAFAO YAPATIKANA MAKABURINI

Inawezekana likawa ni moja ya tukio la nadra kutokea nchini. Alison Mcharo aliyepotea mwaka 2006 imebainika kuwa aliuawa na kuzikwa katika makaburi ya familia yake.
Mcharo aliyekuwa mkazi wa Kijiji cha Mpinji, Kata ya Mamba Myamba wilayani Same, alipotea baada ya kupokea mafao yake ya kustaafu kazi ya ualimu.
Inadaiwa kuwa Mcharo alitoweka baada ya kufika nyumbani na hakuonekana tena.
Jana, Polisi Mkoa wa Kilimanjaro walisema kuwa wamewatia mbaroni mkewe, Nasemba Alison (80) na mtoto wake, Orgenes Alison (45) wakiwatuhumu kwa mauaji hayo.
Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Hamis Issah alisema mabaki ya mwili wa Mcharo yaligunduliwa Jumapili iliyopita, jirani na kaburi la baba yake mzazi.
Kamanda Issah alidai kuwa uchunguzi wa awali uliofanywa na polisi unaonyesha kuwapo kwa ushiriki wa mkewe katika kupanga na kutekeleza mauaji hayo kwa kile alichodai ni tamaa ya fedha.
Haikufahamika mara moja kiasi cha fedha ambacho marehemu alilipwa baada ya kustaafu.
“Uchunguzi wetu wa awali umebaini marehemu aliuawa baada ya kukabidhiwa mafao yake na waliohusika waliingia tamaa baada ya kuona fedha nyingi alizokuwa amekabidhiwa.
“Baada ya kupokea mafao yake na kurudi nyumbani, ndipo aliuawa lakini taarifa ikatolewa kuwa amepotea. Mkewe baada ya kuhojiwa amejieleza vizuri...,” alidai kamanda huyo.
Alisema ripoti ya kupotea kwake ilitolewa polisi mwaka 2006 na kipindi chote cha miaka 12, alitafutwa bila mafanikio hadi Jumapili iliyopita mabaki ya mwili wake yalipoonekana.
Mwili wake uligundulikaje?
Kugundulika kwa mabaki ya mtu anayedaiwa kuwa ni Mcharo kulianzia kwenye kifo cha mama yake mzazi ambaye alikuwa ameacha wosia kuwa azikwe jirani na alipozikwa mumewe.
Kamanda Issah alisema ndugu na jamaa walikwenda kuchimba kaburi eneo ambalo marehemu aliacha wosia, lakini walishtuka kukuta mabaki ya mwili wa mtu mwingine katika eneo hilo.
“Kulikuwa hakuna alama yoyote kama kuna kaburi, lakini cha ajabu walikuta mabaki ya mtu, hapo waliacha kuchimba kaburi na kutoa taarifa Polisi kwa sababu ukikuta kaburi huwezi kuendelea kuchimba.
“Baada ya polisi kupata taarifa hizo tuliomba kibali cha Mahakama na tulipochimba eneo lile, kweli yalionekana mabaki ya mwanadamu na kulionekana kuna tai na shati.
“Hizo nguo zilitambuliwa kuwa ni za mwalimu Mcharo ambaye alidaiwa kupotea na alikuwa hajulikani alipo tangu mwaka, 2006.
“Jambo lingine lililotushangaza tulipofukua kaburi, tulikuta mabaki yale yamekaa mkao ambao si wa maiti inavyozikwa. Ilikuwa kwenye mkao ambao si wenyewe kama taratibu za maziko zilivyo,” alidai Kamanda Issah.
Alisema polisi wanaendelea na uchunguzi wa kisayansi ikiwamo kuchukua sampuli za mifupa ili kuthibitisha kisayansi kuwa ni ndiye.SOMA ZAIDI HAPANa Florah Temba, Mwananchi
2 months ago
Michuzi
NEWZ ALERT: WATU WATATU WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA KUFUATIA AJALI YA 'AMBULANCE' KUGONGANA NA LORI USIKU HUU.

Globu ya Jamii inafuatilia taarifa kamili na sahihi kwa ukaribu kabisa kutoka kwa mamlaka husika.
Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi-Amen


8 months ago
Michuzi
BALOZI WA KUWAIT AKABIDHI VIFAA TIBA KWA HOSPITALI KIGAMBONI

Mapema akimkaribisha mgeni wake, DC Mgandilwa amemshukuru Balozi Najem kwa moyo wake wa upendo kwa watanzania hususani wakazi wa Kigamboni.
Ameeleza kuwa vifaa ambavyo vimetolewa ni vya zaidi ya Shilingi milioni kumi na moja na vinalenga kuondoa changamoto iliyokuwepo katika wodi za akina mama na watoto.
Vifaa vilivyopokelewa ni pamoja na mashine za kusaidia wakati wa upasuaji, mashine za kusaidia kupumua, vifaa vya kupima moyo, vitanda vya watoto na beseni maalum kwa ajili ya akina mama wanaojifungua.
DC Mgandilwa amesema kuwa nchi ya Kuwait ni miongoni mwa nchi ambazo ni marafiki wazuri wa Tanzania na kuwa Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kigamboni itaendeleza ushirikiano huo mwema.

Balozi Jasem ameeleza kuwa vifaa tiba alivyovikabidhi sio msaada bali ni zawadi kutoka kwa watu wa Kuwait kwenda kwa marafiki zao walioko Tanzania.
Balozi Najem ameongeza kuwa huo ni mwanzo tu kwani baadhi ya vifaa tiba vingine vilivyoombwa na DC Mgandilwa atahakikisha vinapatikana na kuletwa ili kusaidia watu wa Kigamboni na watanzania kwa ujumla.
Hafla ya kukabidhi vifaa tiba imefanyika katika hospitali ya Vijibweni na baadae DC Mgandilwa alimkaribisha mgeni wake iftar iliyoandaliwa katika viwanja vya Msikiti wa Gaddafi uliopo Kigambobi.
8 months ago
Malunde10 Jun
MSAFARA WA MWENYEKITI WA UVCCM TAIFA WAPATA AJALI...KUNA TAARIFA YA KIFO

Kamanda wa Polisi mkoani Simiyu, Boniventure Mushongi amesema ni kweli ajali hiyo imetokea lakini anasubiri kupatiwa ripoti kamili.
“Ni kweli taarifa za awali zinasema hivyo, inasemekana kuna basi limeligonga gari lao kwa nyuma” amesema Mushongi.
Katika Ukurasa wake wa Facebook Mkuu wa mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ameandika ujumbe ufuatao.

8 months ago
Malunde10 Jun
MAMA AUA MTOTO WAKE KISHA KUMTUPA MTONI

Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo wamesema kuwa Mwanamke huyo mwenye miaka 23 ambaye anaishi peke yake, baada ya kutenda tukio hilo alimtupa mwanae kwenye mto na kukaa kimya akiamini kuwa maiti ya mtoto wake itachukuliwa na maji na kupelekewa sehemu isiyojulikana.
Aidha mwili wa mtoto huyo umeonekana ukielea katika mto Rutui asubuhi ya jana June 9 na ndipo wakazi wa eneo hilo ikiwemo mtuhumiwa waliwaita Polisi na kuutoa mwili wa mtoto huyo kisha wakamkamata mtuhumiwa.
Kwa mujibu wa Polisi wa kituo cha Kirinyaga Yaya Chome amesema kuwa mwanamke huyo amefunguliwa mashitaka ya kusudio la kutaka kuua katika mahakama ya Kerugoya.
8 months ago
Zanzibar 2409 Jun
Mfanyakazi wa ndani auwa Mama na Mtoto wake
The post Mfanyakazi wa ndani auwa Mama na Mtoto wake appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Zanzibar 2409 Jun
Diamond naye wanataka kumuua -TID
Msanii TID amesema kuwa utaratibu wa wadau/media kushusha wasanii pale wanapodai maslai yao na kuwapandisha wengine ndio kitu kinaathiri muziki wa Bongo Flava.
Muimbaji huyo ameeleza kuwa kitu hicho ndicho kilitokea kwenye muziki wake na kwa sasa kimemtokea Diamond.
“Na kweli anaweza because he has a media, yaani yeye ndio kama Mungu anajiona but mimi hapana. Nilifanya kosa hilo lakini kosa hilo ndilo limewasanua wasanii wengine, unaona msanii kama Diamond naye amekataa,” amesema.
“So Diamond was me lakini wakasema wewe siunajifanya mjanja sasa tunamleta Diamond tukushushe wewe. At the end Diamond naye wanataka kumuua, sijui wanataka kumuweka nani,” TID ameiambia Wasafi TV.
TID ameongeza kuwa hajaona kitu kama hicho nchini Kenya kwani bado anamuona Jaguar ni msanii mkubwa, Nonini ni msanii mkubwa anapewa heshima yake hakuna underground yeyote amewekwa pale kumshusha Nonini.
The post Diamond naye wanataka kumuua -TID appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Malunde09 Jun
HOUSE GIRL AUA MTOTO MCHANGA KISHA KUUA BOSI WAKE

Imedaiwa kuwa mfanyakazi huyo alianza kwa kumpiga mtoto mpaka akamuua kisha akamfuata mama yake na kumchoma kisu mara kadhaa na kisha kumchoma na kitu kinachodhaniwa kuwa ni pasi ya umeme au tindikali.
Kwa sasa jeshi la Polisi Kisumu linamtafuta mfanyakazi huyo ambaye ametokomea sehemu isiyojulikana.
Taarifa zinasema kuwa katika tukio hilo mfanyakazi huyo hakumgusa binamu wa marehemu aliyekuwepo eneo la tukio.
Aidha inasemekana kuwa mfanyakazi huyo alikuwa anaendana kiumri na mwajiri wake kitu kilichokuwa rahisi kwa yeye kutekeleza tukio hilo.
8 months ago
Michuzi
WANAWAKE WASHIRIKI KUJENGA WODI YA MAMA NA MTOTO CHEMBA
Wanawake washiriki kujenga Wodi ya mama na mtoto - Chemba
Wanawake wa Kata ya Songolo, katika Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma wamejitoa katika ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto lililojengwa katika kituo cha afya cha Hamai kilichopo katika Wilaya hiyo kwa lengo la kuchangia nguvukazi ili kupunguza changamoto za kutembea muda mrefu kutafuta huduma za afya.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa kituo hicho Bw. Saidi Msigwa mbele ya timu ya ukaguzi wa ujenzi wa vituo vya afya katika Mkoa wa Dodoma walipokuwa wakikagua maendeleo ya ujenzi wa vituo vya afya mkoani Dodoma.
Amesema kuwa asilimia kubwa ya wanawake wa Kata ya Songolo walijitokeza katika ujenzi wa kituo hicho kwa kuwa ndicho kilikuwa kilio chao cha muda mrefu cha kujengewa Wodi ya mama na Mtoto jambo lililopelekea wanawake wengi hasa wajawazito kwenda kujifungulia katika Hospitali ya Wialaya ya Kondoa.
Amesema kukamilika kwa Kituo cha afya cha Hamai kutasaidia wananchi wengi kupata huduma ya afya hasa vijiji vya jirani ambavyo ni Murongia, Itolwa , Jangalo, Jinjo, Kinkima na Kirerechangombena ambao wote hupata huduma katika kituo hicho.
Bw. Msigwa amesema mwaka 2015 wanawake wa Kata ya Songolo waliamua kijutolea kujenga jengo la Wodi ya Mama na mtoto kutokana na kuwepo kwa jengo moja la wodi ya Mama na Mtoto jambo ambalo lilikuwa likisababisha msongamano wa wamama wajawazito sababu hii ilipelekea wanawake kuamua kuchimba msingi na kukusanya mawe kwa ajili ya ujenzi wa wodi hiyo ndipo serikali ilipoamua kujenga jengo hilo mwaka 2018.
Bw. Msigwa ameishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kujenga kituo cha afya cha Hamai ambacho kitasaidia wananchi maskini ambao walikuwa wakitembea umbali mrefu kwenda kutafuta huduma za afya katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa.Amesema kituo hicho kimejengewa wodi ya mama na mtoto, jengo la upasuaji, maabara, chumba cha kuhifadhia maiti na nyumba ya mtumishi ambapo mpaka sasa tayari zimetumika zaidi ya shilingi milioni 291.
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Charles Kiologwe ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya chemba kwa usimamizi mzuri wa majengo yaliyojengwa ambayo yanaonyesha uhalisia wa matumizi ya fedha zilizotumika ukilinganisha na ubora wa majengo.
Aidha ameutaka uongozi wahuo kukamilisha ujenzi huo kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma za afya katika maeneo ya karibu na wanapoishi.Naye Bi Martha Mariki Afisa afya Mkuu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ameutaka uongozi wa Halamashauri ya Wilaya ya Chemba kuhakikisha maeneo ya taasisi yanapimwa na kuwa na hati miliki, pia kuhakikisha wanaweka kwenye bajeti kama kipaombele cha kuweka uzio wa maeneo ya taasisi ili kuepusha maeneo mengi kuvamiwa na wananchi.




8 months ago
Michuzi
8 months ago
Zanzibar 2408 Jun
Mtoto auawa kwa kuchapwa fimbo na Baba yake kisa kugoma kwenda shule
Jeshi la Polisi katika Wilaya ya Pader, nchini Uganda, linamshikilia Bwana Omony Odokonyero (30) kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mwanae mwenye umri wa miaka saba kilichotokana na kuchapwa fimbo.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor limeripoti Juni 7 2018, katika kijiji cha Omakigira, ambapo mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Richard Odokonyero, mwanafunzi wa shule ya msingi Pader Ogom alipigwa na fimbo baada ya kukataa kwenda shule akitaka kupelekwa kwa bibi yake.
Mwenyekiti wa Kijiji hicho Charles Lalobo, amethibitisha tukio hilo na kudai kuwa mzazi huyo amekuwa na tabia ya kumpiga mtoto wake mara kwa mara na siku ya tukio alikuwa akimpiga na fimbo kichwani hivyo kupelekea kuzimia kabla ya kufariki
“Hili ni tukio ambalo halikupaswa kutokea, kuna njia nyingi za kutumia kama mzazi ili kufundisha watoto wao lakini sio kutoa athabu kali, Polisi wanapaswa kuchukua hatua kali na kuhakikisha mtuhumiwa anaadhibiwa” amesema Bwana Lalobo
Msemaji wa Jeshi la Polisi katika mkoa wa Aswa River, Jimmy Okema, amesema kuwa Jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa katika Makao Makuu ya Polisi Pader na kuongeza kuwa endapo uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani kwa kosa la mauji.
The post Mtoto auawa kwa kuchapwa fimbo na Baba yake kisa kugoma kwenda shule appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Zanzibar 2408 Jun
Wanawake Kaskazini Unguja washajihishwa kujiunga na uzazi wa mpango kunusuru afya ya Mtoto
WAZIRI WA Afya Hamad Rashid Mohammed amewasisitiza akinamama wa mkoa wa Kaskazini Unguja kujishajihisha katika uzazi wa mpango ili waweze kuwa na afya bora na kuweza kuwapatia malezi mema watoto wao.
Hayo ameyasema katika Hospital ya Kivunge wakati alipofanya ziara ya kukagua huduma mbali mbali zinazotolewa katika hospital hiyo ikiwemo huduma ya mama na mtoto.
Alisema ili afya ya mama na mtoto iweze kuimarika ni lazima akinamama wajiepushe na uzazi wa papo kwa papo kwani kufanya hivyo kunaweza kusababisha kuwatokea madhara na kukosa nguvu za kuwahudumia watoto .
Pia amewaomba akina baba kutoa mashirikiano ya dhati kwa akina mama ili waweze kujiunga katika huduma za uzazi wa mpango kwa lengo la kujenga familia iliyo bora yenye afya.
“Natoa wito kwa akinababa kuwaruhusu wake zao wajitahidi kujiunga na uzazi wa mpango na hata dini yetu ya kiislamu inahamasisha uzazi wa mpango kwani mtoto atakuwa na makuzi bora na salama na kuwa na afya njema kwa jamii na Taifa” alisema Waziri huyo.
Ameeleza kufurahishwa kwake kuona huduma mbali mbali zinapatikana katika hospitali hiyo na amewaomba wananchi kutoa taarifa itakapotokea dakatari kumuuzia dawa mgonjwa ili sheria ziweze kuchukuliwa.
Alisema Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohammed Shein ametoa fedha nyingi ili wananchi waweze kufaidika kwa kupata matibabu bure .
Nao Wananchi wa Mkoa huo wamesema wanaridhishwa na huduma zinazotolewa katika Hospitali hiyo ikiwemo huduma ya uzazi salama vipimo na pia walimthibitishia Waziri kuwa madaktari wapo wanatimiza wajibu wao vizuri.
Daktari dhamana wa Hospitali ya Kivunge Tamim Hamadi Saidi amemthibitishia Waziri kuwa hivi sasa wanazo dawa za kutosha na amewataka wananchi wa Mkoa huo wanapopata matatizo ya afya kuendelea kuitumia hospitali hiyo kwani iko katika hali bora kwa dawa.
Na Mwashungi Tahir Maelezo Zanzibar
The post Wanawake Kaskazini Unguja washajihishwa kujiunga na uzazi wa mpango kunusuru afya ya Mtoto appeared first on Zanzibar24.
8 months ago
Malunde08 Jun
BABA AUA MTOTO KISA KAGOMA KWENDA SHULE

Richard odokonyero mwenye miaka 7 alikuwa akisoma katika shule ya msingi Pader kabla ya uhai wake kukatishwa na baba yake Denis Omony Juni 6,2018.
Mwenyekiti wa eneo hilo Charles Otto Lalobo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa baba huyo aligeuka hayawani na kumshambulia mwanae kwa fimbo kichwani kabla ya kufariki.
Inadaiwa kuwa mtoto huyo aligoma kwenda shule kwa kile alichokidai kuwa anatendewa vibaya na mama yake wa kambo na alikuwa akimuomba baba yake ampeleke kwa bibi yake akaishi huko.
Kwa mujibu wa msemaji wa Polisi katika mkoa wa Aswa River Jimmy Patrick Okema amesema kuwa mtuhumiwa huyo ameshikiliwa katika kituo cha Polisi cha Pader na atashitakiwa kwa kosa kuua punde tu upelelezi ukikamilika.
8 months ago
Michuzi08 Jun
8 months ago
Michuzi